Jinsi ya Kutumia Kondom za Kiume na za Kike Kiufasaha..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


NUSU ya watu wanaotumia kondomu kwa ajili ya kujikinga na mimba ama magonjwa ya zinaa, hawajui namna ya kuitumia mipira hiyo

Tumia kondom mpya kila mara unapofanya mapenzi.
Jitahidi kutokugusa sehemu za siri ya mpenzi wako (au osha mikono yako) kabla ya kugusa sehemu zako za siri.

1. Usiguse sehemu za siri za mpenzi wako kabla ya kuvaa kondom. Angalia kwa makini paketi za kondom kabla ya kuifungua.
Hakikisha haijaharibika au kupasuka. 


Angalia tarehe ya mwisho ya matumizi ya kondom hii, ambayo itakuwa imechapishwa sehemu ya nje ya paketi ya kondom kuhakikisha tarehe haijafika. Kama tarehe imeishafika na kupita, tumia kondom nyingine. 

2. Fungua paketi kwa uangalifu kwenye sehemu iliyo na makucha makucha kama msumeno, ili kuhakikisha hauharibu kondom.
Usitumie makucha au meno kufungua paketi, kwa sababu kondom inaweza kuchanika.

Upapogusa kondom, iwe na utelezi kidogo. Kama kondom haina utelezi, imeharibika, kwa hiyo usiitumie. Sehemu ya nje ya kondom huwa na majimaji yanayorahisisha kufanya mapenzi. Kabla ya kuvaa kondom kwenye uume, hakikisha unafahamu sehemu gani inakaa nje unapoikunjua.

Tumia kondom mpya kila mara unapofanya mapenzi.
Usitumie tena kondom iliyokwisha tumika.

3. Weka kondom kwenye uume uliyosimama tu. Minya chuchu iliopo sehemu ya juu ya kondom kuhakikisha hamna hewa ndani yake. Hii ni kuhakikisha kuna nafasi ya kutosha katika kondom wakati mwanaume anamwaga shahawa.

4. Endelea kuminya chuchu na kunjua kondom kwa uangalifu hadi unapofika sehemu ya chini ya uume. Kuminya chuchu kunahakikisha kuna nafasi ya kutosha kupokea shahawa itakayomwagika.
Kama unaweka kondom juu ya uume na unaanza kuikunjua vibaya, usiitumie tena, kwa sababu ukiigeuza kuna uwezekano kuna tone chache za shahawa zilizokaa nje ya kondom.

Usitumie Vaseline, losheni au aina nyingine yeyote ya mafuta kuongeza utelezi wa kondom zaidi. Mafuta ya aina hii huongeza uwezekano wa kondom kupasuka. Kama unahitaji utelezi zaidi, tumia mate au majimaji maalum yaitwayo KY-Jelly, yanayopatikana katika duka ya madawa.

5. Anza kufanya mapenzi

6. Mara tu baada ya kufikia mshindo, toa uume ukeni wakati unaendelea kushikilia kondom kwenye sehemu ya chini ya uume karibu na mapumbu. Kila mara ondoa uume kabla haujalegea kuhakikisha kondom haiachii na kubaki ndani ya uke.

7. Kwa uangalifu, vua kondom kutoka kwenye uume.

8. Funga kondom kwa fundo kwenye sehemu ile ya wazi kuzuia shahawa kumwagika.

9. Funga kondom kwenye karatasi au kwenye paketi yake ya mwanzo.

10. Tupa kondom kwenye choo cha shimo, au ichome moto. Nawa mikono yako na maji na sabuni.

TUMIA KONDOM MPYA KILA UNAPOFANYA MAPENZI.



JINSI YA KUTUMIA KONDOM YA KIKE:
Tumia kondom mpya kila mara unapofanya mapenzi. Kondom ya kike inaweza kuwekwa ndani ya uke mara tu kabla ya kufanya mapenzi, au hadi masaa 6 kabla ya kufanya mapenzi.

Jitahidi kutokugusa sehemu za siri za mpenzi wako (au osha mikono yako) kabla ya kugusa sehemu zako za siri.

1. Tazama paketi ya kondom ambayo bado haijafunguliwa.
Hakikisha haijaharibika au kupasuka.

Angalia tarehe ya mwisho ya matumizi ya kondom hii, ambayo itakuwa imechapishwa sehemu ya nje ya paketi ya kondom kuhakikisha tarehe haijafika. Kama tarehe imeishafika na kupita, tumia kondom nyingine.

2. Fikicha kwa upole paketi ili kuhakikisha majimaji yaliyomo yanasambaa kote kwenye kondom.
Fungua paketi kwa uangalifu kwenye sehemu yenye makucha kama msumeno, ili kuhakikisha kondom haiharibiki.
Usitumie makucha au meno kufungua paketi kwa sababu yanaweza kuchana kondom.

Unapogusa kondom, iwe na utelezi kidogo. Kama kondom haina utelezi, imeharibika, kwa hiyo usiitumie. Sehemu ya nje ya kondom huwa na majimaji yanayo-rahisisha kufanya mapenzi.

3. Ni rahisi zaidi kuingiza kondom ukeni kama unachuchumaa, kupandisha mguu mmoja juu ya kiti, au kulala kitandani ukiwa umekunja magoti wakati umepanua miguu yako wazi kabisa. 

4. Minya kondom kwa nje, ukiminya sehemu mbili za mviringo mdogo wa ndani kwa pamoja kama ilivyooneshwa kwenye picha. Muundo huu hurahisisha kuingiza kondom ukeni.

5. Wakati umeendelea kushikilia sehemu ya nje ya kondom namna hii, pole pole ingiza mduara mdogo wa ndani ukeni ukitumia kidole cha shahada.

7. Hakikisha mduara wa nje wa kondom unaishia kwenye mlango wa uke: usiingie ndani ya uke. Mduara wa nje utafunika mlango wa uke wakati wa kufanya mapenzi. 

8. Usitumie Vaseline, losheni au aina nyingine yeyote ya mafuta kuongeza utelezi wa kondom zaidi. Mafuta ya aina hii huongeza uwezekano wa kondom kupasuka. Kama unahitaji utelezi zaidi, tumia mate au majimaji maalum yaitwayo KY-Jelly, yanayopatikana katika duka ya madawa.

Fanya mapenzi ndani ya muda wa masaa 6 baada ya kuvaa kondom.
Tumia mikono yako kuongoza uume ndani ya kondom, ili kuhakikisha kuwa uume unaingia ndani ya kondom na siyo kando.

9. Baada ya kufanya mapenzi, viringisha mduara wa nje wa kondom mara moja ili kuzuia shahawa kumwagika.
Kisha toa kondom ukeni polepole. 

10. Funga kondom kwenye karatasi au kwenye paketi yake ya mwanzo. 

11. Tupa kondom kwenye choo cha shimo, au ichome moto.
Nawa mikono yako na maji na sabuni.


TUMIA KONDOM MPYA KILA UNAPOFANYA MAPENZI

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad