Kimenukaaa..Nape Aaanzisha Vita na Makonda..Afunguka Mazito Jinsi Ilivyokuwa Hadi Akatumbuliwa..Adai Makonda Anamchonganisha Rais na Wananchi .Amtaka Kuchukua Hatua Haraka..!!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 Kwanza niseme nawapenda sana, nawashukuru sana kwa mapokezi makubwa mliyonipa, Kilichinitoa machozi ni heshma kubwa mliyonipa kina mama. Mlilala chini, mkataka nipite juu yenu, sio jambo ambalo nilitegemea, nawashukuru sana. Niwaahidi nitafanya kazi kwa nguvu zangu zote, kuwatumikieni, usiku na mchana, ntaikumbuka heshima mliyonipa na hio itanisukumu.

Mmenipa heshima kubwa mpaka ntaenda nayo kaburini, pengine sikustahili, upendo wenu umegusa sana moyo wangu. Ntatumia mpaka senti yangu ya mwisho kuhakikisha jimbo la Mtama lina maisha bora. Niwashukuru Steve Nyerere na kundi lake, waandishi wa habari leo wote wamekuja Mtama.

Nilitaka kuongea Dar es Salaam, ikatokea fujo kidogo, Nimeamua kuja nyumbani na leo nitasema.

Mimi ni mtoto wa Kimakonde na nimefundishwa kusema kweli, nimshukuru Rais ambae nilipigana kufa na kupona kuhakikisha anakuwa Rais, nilipata ajali mabya usiku wa manane wakati natoka kutafuta kura. Watanzania wakatupa dhamana na nikapata heshma ya kuwa kwenye baraza la mawaziri moja kwa moja bila kuwa naibu waziri.

Sina mashaka kuwa nilifanya kazi nzuri kwa akili yangu yote kuhakikisha dhamana niliyopewa nameifanyia haki, kama yupo anadhani sikutenda haki asimame hadaharani. Wakati nateuliwa hakukuwa na majadiliano.

Karatasi ukiisoma haina sababu, yalikuwa ni mabadiliko ya kawaida kulingana na Rais. Wakati mwingine ukiwa na mchezaji mahiri na mkafunga magoli ya kutosha, mnampumzisha akacheze tena kesho.

Siku nne au tano kabla ya mabadiliko nilisema mambo kama hayaendi sawa mimi ntajiuzulu. Nilisema kazi hii ngumu na ikithibitika amevamia kituo cha habari, mimi waziri sitatakiwa kubaki madarakani, watu tunatakiwa kuishi kwenye maneno yetu, mimi no mtoto wa mzee Nnauye, ukifika mahali usiyombishwe na cheo.

Kocha ameamua, hakuna sababu ya kumnunia, mechi ikikamata ntarudishwa uwanjani, mimi ni mchezaji bora.

Kwenye sakata hilo kuna mambo ya kipuuzi, haya nitasema. Nikiwa njiani kurudi kutoka Arusha, kuna watu walisema kwenye mitandao Nape amekamatwa, baada ya kukanusha wakaenda kuwaondoa waandishi wa habari hoteleni.

Nilipofika nikakuta waandishi wa habari wamefukuzwa hotelini kwa ubabe, wakaenda nje na mwenye hoteli abaki na hoteli yake. Wakamwaga vijana wengi, nikisema vijana mnawajua. Mimi ninajua, nimekaa miaka 16 ndani ya CCM na nilijua kilichokua kinaendelea na bahati nzuri wanahabari wakaonyesha lile tukio live.

Nilivyofika nikawaona wale vijana, yule kijana mliemuona mpuuzi, akasogea karibu yangu, nikamnong'oneza tuko moja kwa moja vyombo vinaangalia, nikafikiri wana akili, nilisema kulinda sura ya nchi yangu, vyombo vya Dola na Rais wangu. Nilikuwa nasitiri nchi yangu, mpuuzi haoni, nikamwambia niliyonayo ni kubwa kuliko yako, sema nikaona wote tutakuwa wapuuzi.

Nikaingia ndani ya gari na kutoka juu ili aje, ilihitaji busara na nikiwaambia sina nia mbaya. Sikuwa na haja kuharibu kazi ya mikono yangu mwenyewe.


Hivi nani aliweka mguu, Edward asiende mbele? Wao walikuwa kwenye meza ndefu wanakunywa bia wakati wengine tunatafuta kura ndio maana nilikasirika na naamini mtanisamehe kwa kukasirika kwango, mimi ni banadaamu na nina nyongo, nilikumbuka mengi sana.

Kitenndo kilichofanyika hakikuwa cha kiungwana na namshukuru waziri wa mambo ya ndani kusema sina rekodi ya uhalifu.

Nilisubiri wamtafute, na wanasema sio polisi, leo nyoosha bastola hewani uone kama polisi hawajaondoka na wewe na pale alikuwepo RPC.

Siamini kama alitumwa kuonyesha silaha, mimi ukinitolea silaha naoa kama mic tu. Shida niliyonayo huyu jambazi alietoa silaha, vyombo vya ulinzi na usalama vinafanya nae nini. Kama wameweza kumfanyia Nape, watanzania wangapi watafanyiwa huku mitaani. Vingenevyo wataonewa wengi, naamini wako wengi wametolewa huko, Kijana mmoja wa CHADEMA, Ben Saanane amepotea kwa miezi mingi, watu wamevamia kituo na wameonekana, tusema alieonekana sie yeye, nani alieagiza mtu akiwa na vyombo vya ulinzi na usalama kuvamia studio. Matukio haya yanawafanya watu waishi kwa hofu

Dar imevamiwa studio akiwemo Roma Mkatoliki, sikwenda CCM kwa sababu mzee Nnauye yuko CCM, nilienda CCM kwa sababu ya imani ilikuwa CCM, sema kweli fitna kwangu mwiko.

Kazi ya msingi ya kikatiba ya serikali, ni kulinda raia na mali zao, ombi langu kwa serikali na Rais aunde tume huru iyachunguze matendo haya ili yasijirudie tena. Mimi nimewasemehe ila haya matendo mengine, yanamjengea chuki yeye(Rais) na wananchi kwa sababu wanadhani ni yeye ndie anaewatuma.

Matendo haya yanachonganisha CCM na wananchi, huko mtaani watu wanasema, namshauri kama mwenyekiti wa chama changu, watu wachche wanaotumia mamlaka waliyopewa kuumiza watu, lazima tume iiundwe.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Ni askari na ndiyo maana wameipuuza koz walijua kila kitu

    ReplyDelete

Top Post Ad