Lulu Atokwa Povu Bethidei Yake Kubuma...!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Kweli utawala wa awamu ya tano kiboko! Tofauti na miaka iliyopita ambapo mastaa mbalimbali hufanya kufuru katika kusherehekea kumbukumbu ya siku zao za kuzaliwa, Jumapili iliyopita, ambayo ilikuwa ni bethidei ya staa wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’, lakini haikufanyika

Chanzo makini kilipolidokeza Risasi Mchanganyiko juu ya kutofanyika kwa shughuli hiyo, liliwasiliana na muigizaji huyo, lakini katika hali ya kushangaza, alitoa povu (kufoka) mno, akitaka watu kuachana na habari zake, kwa vile haziwahusu. Kwa miaka kadhaa iliyopita, Lulu alidhimisha bethidei yake katika hoteli kubwa au kumbi zenye ‘akili’ zikiambatana na mbwembwe nyingi za ulaji na manywaji, lakini mwaka huu imekuwa kimya.

“Mwaka huu Lulu hajafanya sherehe kama ilivyozoeleka miaka mingine iliyopita, hapo ndiyo unajua kiukweli mambo yamebana awamu hii, hakuna fedha, bethidei yake imebuma, hakuna cha ukumbini wala nini, hapana chezea utawala wa Rais Dkt. John Magufuli, kila mtu ana nidhamu ya fedha,” kilisema chanzo hicho.

Ili kuujua ukweli, Risasi Mchanganyiko lilimtafuta kwa njia ya simu Lulu ili kumsikia anazungumziaje kuhusu siku yake hiyo kubwa maishani mwake.

Risasi: Haloo Lulu, gazeti la Risasi hapa, hongera kwa kuongeza mwaka mwingine kwenye maisha yako.

Lulu: Asante sana.

Risasi: Je, bethidei yako ulifanyia wapi maana mashabiki wako wanapenda kujua ilikuwaje?

Lulu: Hilo haliwahusu.

Risasi: Kuna habari kwamba mwaka huu hujafanya sherehe kwa sababu ya ukata, hili likoje?

Lulu: Kama nimefanya au sijafanya linawahusu nini, kwanza kuanzia leo msinipigie simu tena, yaani sitaki kabisa simu zenu.

Risasi: Sisi tulitaka tu kuujua ukweli kuhusu suala la kwamba ukata ndiyo umesababisha sherehe isifanyike.

Lulu akakata simu.

Hata hivyo, wakati Lulu akishindwa kufanya sherehe hizo Jumapili, jana yake, msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya, Isabela Mpanda, alifanya bethidei yake katika Ukumbi wa Belinda uliopo Mbezi Beach.


----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Na haramu imebumba awamu hii na ndio maana wanaharamu hawaipendi awamu ya tano.

    ReplyDelete

Top Post Ad