Watu Wangu Wote Wamenitosa - TID Afunguka

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Watu wangu wote wamenitosa - TID


Msanii wa muziki wa kizazi kipya TID Mnyama amefunguka na kusema sasa hivi watu ambao mwanzo walikuwa wakimpa support kwenye muziki na mambo yake mengine wamemtosa na hawampi msaada wowote hivyo kila kitu anapambana mwenyewe. 


TID amesema hayo kwenye kipindi cha Planet Bongo ya East Africa Radio na kusema watu hao wameacha kumpa suport baada ya yeye kuachana na madawa ya kulevya hivyo saizi wao wanamuona yeye ni kama msaliti.


"Saizi kila kitu nafanya mwenyewe hata hao mabrother unaosema washanitosa maana wao walikuwa wanapenda kuona nazidi kuharibika, hivyo toka nimetangaza kuachana na madawa ya kulevya wao wananiona mimi kama 'snitch', lakini hilo halina tatizo kwani mimi mwenyewe niko vizuri ndiyo maana unaweza kuona video hii nimetumia pesa nyingi kuifanya na nimelipa mwenyewe, hii pesa ningesema ninue gari basi ningepata Mark X nyingine lakini nimeamua kuiweka kwenye video ili kuleta ubora zaidi" alisema TID 


TID leo ameachia ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la 'Woman' na kusema siku yoyote ataachia video ya ngoma. 
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hiyo sijida usoni inakusuta.rudi kwa ALLAH kabla hujarudishwa kwa ALLAH.

    ReplyDelete

Top Post Ad