CONFIRMED: Ni Kweli Tanzania Imenunua Ndege ya Boeing 787-8 Yenye Line Number 719..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Kumekuwepo na uvumi kuwa eti Tanzania imenunua ndege mbovu aina ya boeing 787-8 Dreamliner ambayo ni Terrible Teen line number 19 yenye serial number 35508.

Uvumi huo na uchochezi huo ulienezwa na kukolezwa zaidi na mbunge wa Kigoma mjini mh. ZK kwenye mitandao yake ya kijamii zikiwemo akaunti zake za facebook na twitter kuwa eti serikali imenunua ndege TT liyokatataliwa na Rwanda na Moroko yenye line #19 kwa bei ya ndege mpya na ZK kupata uungwaji mkono wa watanzania wengi.

Mh. ZK amekuwa akitoa ushahidi kutoka vyanzo visivyo na uhakika kama b787register.com, chanzo ambacho kimeweka taarifa kuwa ndege hiyo itakuwa delivered kwa Air Tanzania mwezi Agosti 2017 kitu ambacho ni uongo.

Ikumbukwe kuwa baada ya mazungumzo kati ya Rais wa Tanzania na Mkurugenzi wa Masoko ya Afrika wa Kampuni ya ndege ya Boeing Bw. Jim Deboo, Rais wa Tanzania alisema kuwa ndege inayonunuliwa na Tanzania itawasili mwezi juni mwaka 2018.

Katika majibu yake bungeni kwa swali lililoulizwa na mh.ZZK , waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Mbarawa alikanusha uvumi kuwa Tanzania imenunua ndege ambayo ni Terrible Teen yenye line#19 na kubainisha wazi kuwa taarifa hizo ni za uongo na ukweli ni kwamba ndege ya boeing 787-8 iliyonunuliwa na Tanzania ni mpya kabisa na ina line #719 .

Sijui kwa kutafuta kick zaidi, mh ZK akazidi kutweet kuwa eti Mh Waziri amedanganya bunge anaficha ukweli na hata mh mbunge huyo kutweet akiwauliza Boeing kuhusu TT line #19 kuuzwa kwa Tanzania kwa bei ya mpya, uzuri Boeing hawakumjibu.

Sasa imekuja kudhihirika kuwa maneno ya Waziri ni sahihi kuwa Tanzania imenunua ndege mpya ya Boeing 787-8 yenye line #719. Ndege 787-8 TT yenye line #19 imechukuliwa na kampuni nyingine

Woodys AeroImages na 787blogger kupitia akaunti zao za twitter wamethibitisha kuwa ndegeiliyonunuliwa na Tanzania kutoka Boeing ni yenye line #719

My Take: Nawashauri wanasiasa wasiingize siasa katika mambo ya msingi ya maendeleo ya Taifa kwa ajili ya manufaa yao kisiasa, hiyo inaweza kuwaharibia na wakati mwingine kupoteza imani kwa wananchi
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Takadiri kama hujafanya utafiti usitoe comment vinginevyo utakuwa unalenga kupotosha wasiojua

    ReplyDelete

Top Post Ad