KWA Mwendo Huu Ninamhurumia Maalim Seif na CUF Zanzibar!..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mzee Kikwete hupenda kusema, ‘’akili za kuambiwa, changanya na zako’’.

Maalim Seif na wapambe wake wa Zanzibar walikubali akili za kuambiwa lakini hawakuchanganya naza kwao.

Maalim Seif hakufahamu kuwa washauri wake wakubwa ni CCM B ambao hawakumtakia mema na kama alifahamu basi alitakiwa achukue ushauri wao na kuchanganya na akili zake.

Kama angechanganya na akili zake kwa sasa CUF isingekuwa katika hali iliyopo kwa sasa. CUF ya kabla ya Uchaguzi Mkuu 2015 sio hii ya leo ambayo inagawana vito kila siku.

Kwa sasa amezunguka dunia nzima akipiga kelele kuhusu kuibiwa kura huku akiwaaminisha wapambe wake yuko mbioni kuingia Ikulu ya Zanzibar kabla ya 2020 lakini ukweli unazidi kumsuta kila siku.

Baada ya kuzunguka dunia nzima kwa sasa amehamia mpaka kwa wachungaji kama Josephat Gwajima kama mentor wake. Hii ni dalili inayoonyesha desperation and kicking a dead horse.

This is an enormous leap for Maalim Seif, catapulting him to a new level of obscurity.

Kinachofanywa kwa sasa na UN, EU wakisaidiwa na Marekani kinatoa maandiko ukutani kuwaambia wale ambao wanadhani Maalim Seif ataingia Ikulu ya Zanzibar kabla ya Uchaguzi Mkuu 2020 wasipoteze muda wao.

Ieleweke kuwa fimbo ya kuichapia serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilikuwa ni kuinyima misaada au kuweka shinikizo kubwa kwa serikali ya Tanzania. Kinachofanyika kwa sasa ni kinyume chake kwa maana nyingine, Wazungu wanamwambia Maalim Seif, Let bygones be bygones.

Ninatumaini Uchaguzi Mkuu ujao, Maalim Seif atachangaza na akili zake baada ya kura kuanza kuhesabiwa.

Hii sio dalili nzuri kwa Maalim Seif na CUF Zanzibar.

Waingereza husema, ‘’Sometimes you’ll never know the value of what you have until it’s gone’’.

Nimalize kwa kusema, A Chinese military general, strategist and philosopher, Sun Tzu once said, If you know the enemy and know yourself, you need not fear the result of a hundred battles. If you know yourself but not the enemy, for every victory gained you will also suffer a defeat. If you know neither the enemy nor yourself, you will succumb in every battle.

Source - Jf
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad