MAUAJI..Kada wa CCM Auawa kwa Kupigwa Risasi bele ya Familia Yake Mkoani Pwani ,Kibiti..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kata ya Bungu wilayani Kibiti, Alife Mtulia ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana akiwa nyumbani kwake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga amesema mauaji hayo yamefanyika usiku wa kuamkia leo (Jumapili) katika Kijiji cha Nyambunda.

Amesema Mtulia aliuawa na watu hao alipokuwa anakwenda kuoga.Kamanda amesema mwili wa marehemu umepelekwa kituo cha afya cha Kibiti kwa uchunguzi.

Mauaji ya askari Polisi, viongozi wa Serikali za Mitaa na raia yamekuwa yakifanyika mara kwa mara katika wilaya za Kibiti, Rufiji na Mkuranga mkoani Pwani.

Jumanne wiki hii akiwasilisha bungeni bajeti ya wizara yake, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba aliliambia Bunge kuwa Serikali itaanzisha mkoa mpya wa kipolisi katika wilaya za Kibiti, Rufiji, Mkuranga na Mafia. Utaitwa mkoa wa kipolisi Rufiji.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad