AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Watu 19 wameuawa na wengine 50 kujeruhiwa baada ya bomu kulipua ukumbi wa tamasha la muziki, katika mji wa Manchester, Uingereza.
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May ametaja tukio hili kama kitendo cha ugaidi.
Iwapo shambulio hilo litathibitishwa kuwa ni la kigaidi, linatajwa kuwa ni baya zaidi kuwahi kuikumba Uinereza.
Shambulio kubwa zaidi lilitokea Julai 2005 ambapo watu zaidi ya 50 walipoteza maisha baada ya kutokea mlipuko, jijini London.
Katika tukio la jana, mashuhuda wanasema shambulio hilo lilitokea mara tu baada ya mwanamuziki wa Marekani Ariana Grande kumaliza kuwatumbuiza mashabiki wake.
Mashudhuda wa tukio hilo wamesema waliona misumari iliyotapakaa sakafuni na harufu ya mabomu.
Eneo kulikotokea mulipuko huo limezingirwa na polisi waliojihami wanaendelea kushika doria.
Wakati huo huo Waziri Mkuu Theresa May anatarajiwa kuongoza kikao cha dharura cha kamati ya usalama baadaye leo.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK