AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Vigogo wa soka nchini, Simba na Yanga watachuana na timu za Kenya kusaka bingwa wa Ligi ya SportPesa Super Cup.
Ligi hiyo itaanza Juni 5 ambapo Yanga itafungua dimba na bingwa wa Ligi Kuu ya Kenya, Tusker siku hiyo pia kutakuwa na mchezo kati ya Singida United na AFC Leopards.
Juni 6, Simba itaonyeshana uwezo wa soka na Nakuru All Stars wakati na Gor Mahia itacheza na Jang'ombe ya Zanzibar, mechi zote zikichezwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji wa SportPesa Tanzania, Abass Tarimba alisema mashindano hayo yataendeshwa kwa mtindo wa mtoano na fainali itachezwa Juni 11.
"Bingwa ataondoka na kitita cha Dola 30,000 na mshindi wa pili Dola 10,000 na timu zitakazoingia nusu fainali kila moja itapewa Dola 5,000 na timu zote zitakazoshiriki zitapewa kifuta jasho cha Dola 2,500 kila moja," alisema Tarimba.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK