UKWELI Mchungu..Siku Zinavyozidi Kwenda Inaonesha Kuna Uhaba Mkubwa wa Wanaume Nchini Serikali Iangalie Jambo Hil..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


kutokana na matukio kadhaa yanayoendelea ni wazi kuwa nchini kuna tatizo kubwa sana la upungufu wa wanaume(UWAWA) hasa Mafaru Dume. nimekuwa nikikaa na vijana sehemu mbalimbali na kuasikiliza maneno yao na kuangalia matendo yao siku za weekend kiukweli nimekatishwa tamaa sana. kuna mambo ambayo kama vijana kuna haja ya kukumbushana maisha haya dada zetu watakuja kukosa watu wa kuwaoa kabisa.

1. mtu unamkuta ana lalamika, anasononeka na kunung'unika kwa mambo ya kipuuzi kabisa hatafuti ufumbuzi yeye kila siku anasema maisha magumu na asilimia 70 ya maongezi yake ni kuhusiana na wanawake au wanaume .. nani anatoka na nani au nani ana beef na nani. hatukuwa na team x na team y.hayo mambo hayakuwepo.

2. unakuta mtu amevaa suruali au kaptula lakini maongezi yaliyomjaa ni kuponda wenzie wanavyofanya au wanavyokula na kuvaa. sisi zaman ilikuwa ukifanya hivyo kama ni kijiweni wanakufukuza haraka sana wanakwambia hiyo si sehemu yako

3. unakuta mtu kavaa suruali kabisa au kaptula na jina la kiume anasimulia alimtembelea mwenzie sehemu akakuta mwenzie analala chini au hana kitanda na pengine akasema jamaa anapikia jiko la mkaa au kila siku anakula mihogo. hii miaka yetu tunakua usingeweza isikia kabisa.

4. unakuta jamaa kavaa nguo za kiume amesimama au amekaa sehemu na kuna mwanamke ananyanyaswa au mtoto ananyanyaswa na huyu naye amesimama au kukaa sehemu hiyo kana kwamba yeye haimhusu. miaka yetu sisi tulikuwa tunapoona mwanamke au mtoto ananyanyaswa tuna chukua nafasi zetu za uanamue au ubaba haraka sana pasipo kusita.

5. unakuta kajikajana kamepishana na mwanamke kanapiga miruzi au makelele.sisi zaman hatukuwa tukifanya hivyo. ni mawili unamfuata kumsemesha na kumpa sifa zake au unakula kona kama vile hujamwona unamsifia kimoyo moyo

6. miaka ile ilikuwa ngumu kabisa kumwona mtu anaonesha chupi aliyovaa au boxer kwa kuvaa mlegezo . na mtu wa hivyo asingeruhusiwa kukaa na wanaume kijiweni maana wangedhan anajihusisha na mambo haramu.siku hizi eti ni fashion moja wapo

7. miaka yetu ilikuwa huwezi kaa kwenye daladala na kuna mwanamke mjamzito au mtu mzima amesimama wewe ukawa unachezea chezea simu au unasikiliza music. ilikuwa ngumu.wanaume tulikuwa makamanda na tuna kazi ya kuilinda jamii na kuisadia kila wakati.

8. hatukuruhusu ulalamishi na kulia lia kwa mtu ambaye tunadhani ni mwanaume. ilikuwa haitokei, watu tulikuwa tunakomaa na changamoto kwa hali na mali. ilikuwa huwezi sikia mtu anatukana badala ya kutoa hoja. ilikuwa uanaume ni kupambana na kusaidia jamii kwa ujumla. hatukuwa na ubinafsi. jamaa yako kama hajala ukinunua chakula mnakula wote.ilikuwa kama jamaa amekosa kitu flan unamsaidia apate. na kama mwanaume mwenzie amekosea jambo unamwambia na yanaishia huko huko huji kutangaza kwa wanaume wenzio. na ilikuwa ukiletea habari kuwa "flan ana....." ukamsema negatively sisi wanaume wengine tungekubalasa uondoke hufai kukaa na wanaume ukiwa unawasema wenzio vibaya.

9. ulaji wetu ulikuwa ni mzuri tunapiga msosi hasa sababu kila kazi ambayo ilikuwa inapaswa ifanywe nasi tuliifanya. ilikuwa ukifika wakati wa kula miaka ile tunakula chakula cha kutosha sana. na tukimaliza tunashushia maji mengi au maziwa. hatukuwa tukijivunga wakati wa kula.tofaut na sasa mtu anakula ugali mdogo,chips au sausage.

10. sisi tulikuwa na miili iliyojengeka vizuri sana ya ukakamavu. hatukuwa wazembe wa kujipodoa na kuwa lege lege. ilikuwa ni ngumu kusikia unamwita mwanaume mwenzio "we fala" au "ms**g* ugomvi wake ungekuwa mkubwa sana ingekuwa issue hasa. na haikuwezekana kabisa kwa mwanaume kumshika mwanaume mwenzie makalio. maana huyo uliyemshika angeweza kukupiga na kitu chochote kilicho karibu na hakuna ambaye angekutetea hata kama ungekufa au kujeruhiwa vibaya. maisha ya sasa yamebadilisha sana watu.

tunakoeleka nadhan mambo yatakuwa mabaya sana. kama nawe kuna mambo ambayo unayaona si ya ki uanaume kwa sasa yaweke tu hadharani ili tuliokoe taifa hili.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Wenyewe wanajiita kizazi kipya sasa mimi huwa najiulizaga kwa mambo yapi mapya?Huwa sipati jibu....

    ReplyDelete
  2. kuuiga tamaduni za watu wengine ndio chanzo.halafu munaambiwa ustaarabu.
    USTAARABU ULIKUWA NA BABU ZETU NA BIBI ZENU.mapenzi mpaka kufa sio leo pochi ikisha mapenzi yanayumba yumba.

    ReplyDelete

Top Post Ad