Baada ya siku 45, Hatimaye Aliyeuawa na Polisi kwa ‘Ujambazi’ Azikwa Dar

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwili wa denti wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Marehemu Salum Almas aliyeuawa kwa kupigwa risasi na polisi kwa madai kuwa alikuwa Jambazi, Mei 14, mwaka huu maeneo ya Uhamiaji Kurasini jijini Dar, ukiwa umebebwa tayari kwa kuzikwa katika makaburi ya Kisutu Jijini Dar.

HATIMAYE mwili wa denti wa UDSM (Chuo Kikuu cha Dar es Salaam), Marehemu Salum Almas aliyeuawa kwa kupigwa risasi na polisi kwa madai kuwa alikua jambazi, Mei 14 mwaka huu, maeneo ya Uhamiaji Kurasini jijini Dar es Salaam, leo Ijumaa Julai 30, 2017 umezikwa katika makaburi ya Kisutu jijini Dar amba mamia ya watu walijitokeza, ikiwa ni siku 47 tangu auawe kwa tuhuma hizo, ambazo familia ya marehemu imezipinga vikali mahakamani kuwa ndugu yao hakuwa jambazi na kulitaka Jeshi la Polisi kukiri kosa.

Mwili wa Denti huyo wa UDSM uligomewa kuzikwa na ndugu zake kwa madai kuwa aliuawa kimakosa kwa kudhaniwa ni jambazi aliyetaka kupora fedha kwenye ATM iliyopo maeneo ya Uhamiaji, Kurasini jijini Dar. Mwili wa Marehe,mu uliswaliwa katika Msikiti wa Kichangani, Magomeni, Dar mara baada ya swala ya Ijumaa. Hapa chini nimekuwekea picha 12 za msafara kuelekea makaburini.

VIDEO: Familia yasusia maiti jeshi la Polisi Dsm
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad