Mhe Mghwira Siachii Uenyekiti wa ACT Ng'oo,Mbona Mbowe Ni Mwenyekiti wa Chama na Pia ni Mbunge...!!!!?

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


MKUU wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira amesema hana mpango wa kuachia nafasi yake ya uenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo.


Mghwira alitoa msimamo huo baada ya kuapishwa kushika wadhifa huo na Rais Dk. John Magufuli Ikulu, Dar es Salaam jana.

Alisema kwa sasa anachokiangalia ni kusimamia shughuli za maendeleo kwa faida ya Watanzania.

Juni 3, mwaka huu, Rais Dk. Magufuli alimteua Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, uteuzi ambao ulizua maswali na mshtuko mkubwa katika tasnia ya siasa.

Mjadala mkubwa uliibuka kutokana na cheo alichopewa, kuwa ni tofauti na kile cha ubunge, huku wengine wakienda mbali zaidi huenda kuna usaliti.

Mghwira ambaye katika uchaguzi mkuu wa mwaka juzi, aligombea urais kupitia ACT- Wazalendo, sasa atalazimika kusimamia utekelezaji wa ilani ya CCM.

Mbali na hilo, pia atabeba jukumu la kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa.

MGHWIRA

Akizungumza jana, Mghwira alieleza kushangazwa na namna watu wanavyohoji endapo ataachia uenyekiti wa ACT-Wazalendo, wakati kuna mambo ya msingi.

“Sasa unataka niseme nini wakati leo (jana) ndio nimeapishwa? Hakuna vitu vya msingi vya kuhoji?  Mimi sitazami hizo nafasi.

“Mimi ni mwenyekiti wa chama na kama unakumbuka wakati Magufuli aliposhinda urais, nilimkabidhi ilani ya chama chetu na hata leo (jana) wakati ananikabidhi ya CCM nilimkumbusha kuwa hata mimi nilimpatia ya ACT akasema kweli anayo.

“Lakini kwani tatizo liko wapi? Mbona Mbowe (Freeman) ni Mbunge wa Hai halafu ni Mwenyekiti wa Chadema sasa tatizo liko wapi kwangu?” alihoji.

Alipoelezwa na mwandishi kuwa upo utofauti wake na Mbowe kwa kuwa yeye anakwenda kutekeleza ilani ya CCM, alisema. “Bungeni wanatekeleza ilani ya chama gani? Waziri Mkuu na wengine wote wanatekeleza ilani ya chama gani?

“Nikwambie tu, wengine ni maneno tu hawasomi hata hii ilani ya CCM na kwamba ilani yao si mbaya kinachotakiwa ni utekelezaji tu,”alisema.

Alisema chama chochote kinapoingia madarakani hakuna mbadala zaidi ya kutekeleza ilani yake.

“Mara nyingi tumekuwa tukilalamika ooh tunaonewa, tukipewa huo uhuru tena tukatae? Tujikite kwenye masuala ya msingi,”alisema Mghwira.

Kuhusu kipaumbele chake katika Mkoa wa Kilimanjaro, alisema ataanzia pale alipoishia Said Meck Sadick na kwamba ataripoti eneo lake la kazi ndani ya wiki hii.

Alipoulizwa endapo kabla ya kuapishwa amekutana na viongozi wa chama chake, alisema. “Jana tumeongea sana na viongozi wangu na leo (jana) tutaonana,” alisema.

Credit - Mtanzania
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. hongera mama kwa kupata nafasi ya kuwatumikia wana kilimanjaro

    ReplyDelete

Top Post Ad