AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mtendaji wa kijiji cha Kinenulo Martini Mwalongo amesema kuwa chanzo chamoto huo hakijajulikana na kwamba moto huo umetokea wakati wanafunzi wakifanya ibada katika vyumba vya madarasa huku milango na madirisha katika mabweni yaliyo ungua vikiwa yamefungwa.
Baadhi ya wanafunzi wameiambia ITV kuwa mabweni yaliyoungua ni matatu yote yakiwa ni ya wavulana huku wazazi wakiiomba serikali kuhakikisha chanzo cha moto huo kinafahamika haraka.
Katibu tawala wa mkoa wa Njombe Jackson Saitabau amefika shule ya sekondari Philip Mangula mapema asubuhi na kuagiza wanafunzi kuendelea na masomo na kwamba halmashauri ya wilaya ya Wanging'ombe kwa kushirikiana na ofisi ya mkuu wa mkoa wakiendelea kufanya tathmini ya mali zilizoungua na vikiwemo vifaa vya wanafunzi.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK