EDWARD Lowassa Aweka Wazi Mikakati yake ya Urais Mwaka 2020

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Edward Lowassa amesema kuwa licha ya kuwa upinzani nchini Tanzania unakumbwa na changamoto nyingi, lakini atagombea tena urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Lowassa amesema kuwa atagombea tena na kwa mapenzi ya Mungu anaamini kuwa atashinda na kuingia Ikulu kwa mikono safi.

Lowassa ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa Nation Media Group (NMG) jijini Nairobi, Kenya.

“Kwa mapenzi ya Mungu nitajaribu tena mwaka 2020 na nitapita kwa mikono safi,”  alisema Lowassa.

Kwa mwaka 2015, Lowassa aligombea urais kwa tiketi ya CHADEMA akiungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) na kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), alipata kura  6,072,848 sawa na asilimia 39.97 ya kura zote halali.

Lowassa alishindwa na Rais Magufuli ambaye alikuwa akipeperusha bendera ya Chama cha Mapinduzi (CCM) aliyejizolea kura 8,882,935 sawa na asilimia 58.46.

Katika uchaguzi huo uliopita Lowassa aliukosoa na kusema kuwa aliibiwa kura zake. Aidha, alifafanua kuwa, licha ya kuwa uchaguzi huo haukuwa huru na wa haki, bado anamtambua John Pombe Magufuli kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Hata kama Dk Magufuli alichaguliwa katika mfumo usioaminika wa uchaguzi, bado tunamheshimu kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Utendaji wa Rais Magufuli utaamuliwa na watu utakapofika mwisho wa muhula huu mwaka 2020. Bora niwe makini katika hili nisije nikanukuliwa vibaya nikaingia kwenye matatizo nitakaporudi nyumbani,” alisema Lowassa

Kuhusu kuzuiwa kwa mikutano na maandamano ya kisiasa, Lowassa alisema kuwa watakwenda mahakamani kuishtaki serikali kufuatia zuio hilo kwani ni kinyume na sheria. Alisema kuwa, watu zaidi ya milioni 6 walimpigia kura, lakini kitu cha ajabu haruhusiwi hata kwenda kuwashukuru.

“Nilipata kura milioni sita na siwezi kufanya mikutano hata ya kuwashukuru watu kwa kunipigia kura. Hiyo si tu kinyume cha demokrasia, bali si haki.”

Lowassa alikwenda Kenya kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa Waziri wa Usalama, Jenerali Joseph Nkaiser aliyefariki hivi karibuni.

Mbali na siasa za Tanzania, Lowassa aliwasihi wa Kenya kufanya uchaguzi kwa amani na kuepuka vurugu kama za mwaka 2007 ambazo zilipelekea zaidi ya watu 1000 kufariki dunia, huku maelfu wakijeruhiwa pamoja na mali na miundombinu kuharibiwa vibaya.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Na ndoto zake za mchana mchana mmmmmhh. Michosho tu

    ReplyDelete
  2. Ana uhakika kwamba LAZIMA chadema watampitisha yeye, kwani 'MPUNGA' alotoa kwa 'mbadilishia-gea-angani' sio wakitoto, hawezi kukwepa, chama alishauziwa zaamaanii....hahaha UKISTAAJABU-YA-CUF-UTAYAONA-YA-CHADEMA

    ReplyDelete

Top Post Ad