Rais Kikwete Akosoa Wanaozuia Watu Kwenda Kutibiwa Nje ya Nchi.......!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Rais Mstaafu, Dkt Jakaya Kikwete jana aliibuka na kutolea utetezi kufuatia Benki ya Dunia (WB) kukosoa serikali za nchi za Afrika Mashariki namna zinavyoshughulikia maendeleo ya sekta ya afya, na jinsi viongozi walivyoshindwa kuboresha huduma hiyo muhimu kwa jamii, huku wao wakisafiri kwenda nje kutibiwa.

Akizungumza katika ufunguzi wa watoa huduma za afya, wamiliki wa vituo vya afya na wataalamu wa afya kutoka nchi za Afrika Mashariki na nje ya Afrika, Rais Kikwete alisema kuwa, kusimama kwenye majukwaa na kusema kuwa, watu kwenda kutibiwa nje ya nchi ni kupoteza fedha, jambo hilo si sahihi.

Alisema, serikali za Afrika Mashariki zimekuwa zikijitahidi sana kuhakikisha zinaboresha sekta za afya, lakini akatahadharisha kwamba, maendeleo ya kiwango cha juu kama nchi zilizoendelea hayawezi kupatikana kwa usiku mmoja.

Akieleza sababu kubwa inayopelekea watu kwenda kutibiwa nje ya nchi, Rais Kikwete alisema ni kutokana na upungufu wa wataalamu katika nchi hizo. Akitolea mfano Tanzania ambapo kuna wataalamu watatu wa upasuaji wa mishipa ya fahamu ambapo kwa kawaida hawawezi kuwahudumia wananchi ambao ni milioni 50.

Rais Kikwete aliisihi Benki ya Duania (WB) kutumia suala hilo kama changamoto kwa kuziwezesha nchi za Afrika Mashariki kuboresha sekta ya afya badala ya kutoa lawama kwamba serikali hazifanyi jitihada jambo ambalo si sahihi. Wananchi wanalalamika, sasa na wewe (mwakiliashi wa WB) hautakiwi kuwa katika nafasi ya kulalamika bali kuhakikisha fedha za kuboresha sekta ya afya zinaletwa, alisema Rais Kikwete.

Akizungumza kabla ya Rais Kikwete, mwakilishi wa WB, Khama Rogo alionyesha kushangazwa na wananchi wa nchi hizo kupoteza maisha kutokana na magonjwa kama vile, malaria, kutapika, kuharisha huku viongozi wa nchi hizo wakienda kutibiwa nje ya nchi.

Rogo alisema mara nyingi huwa anasikia viongozi wa Afrika wamekwenda kupatiwa matibabu nje ya nchi jambo ambalo yeye linamkera kwani anaona badala ya wao kuimarisha miundombinu ya ndani wanapoteza fedha nyingi kwenda kutibiwa nje ya nchi. Katika hali ya masikitiko, alisema, mara nyingi anaposikia suala la afya kutoka nchi za Afrika, ni mtu amefariki.

Mkutano huo uliohudhuriwa na nchi 12 pia ulituma ujumbe wa wahudumu katika sekta ya afya, kutoa huduma sahihi na kwa wakati ili kuweza kupunguza vifo vinavyoepukika.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Eti "rais Kikwete" (title yako hapo juu )uwe makini next time au unabahatisha nn na vyeti vya kibashite

    ReplyDelete

Top Post Ad