Korea Kaskazini Yarusha Makombora Baharini

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Korea Kaskazini Yarusha Makombora Baharini
Korea Kaskazini imerusha makombora matatu ya masafa mafupi , jeshi la Marekani limesema.
Makombora hayo yalirushwa kutoka eneo moja katika mkoa wa kaskazini wa Gangwon na kuruka kwa umbali wa kilomita 250 kulingana na maafisa wa Korea Kusini.

Tangu ifanyie majaribio kombora lake la masafa marefu mwezi uliopita, Pyongyang imetishia kurusha makombora yake katika kisiwa cha Marekani cha Guam.
Lakini jaribio hili la hivi karibuni linajiri kufuatia zoezi la kijeshi la pamoja kati ya Marekani na Korea Kusini.

Maelfu ya wanajeshi wa Marekani na Korea Kusini wanaendelea kufanya zoezi la pamoja ambalo hufanywa kwa kutumia Komyupta.

Marekani awali ilikuwa imeripoti kwamba makombora mawili yalikuwa yamefeli , lakini kulingana na tathmini yake mojawapo ya makombora hayo lililipuka wakati huohuo liliporushwa huku mengine mawili yakiruka kwa umbali wa kilomita 250 yakielekea maeneo ya kaskazini mashariki.
Makombora hayo yalirushwa kwa tofauti ya dakika 30 , kulingana na afisa mmoja.
Wizara ya ulinzi ya Korea Kusini ilisema: Jeshi linaangalia kwa umakini hatua ya Korea Kaskazini ya uchokozi.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad