Makati Ulivyoandaliwa Kumng'oa Maalim Seif CUF Washtukiwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Makati Ulivyoandaliwa Kumng'oa Maalim Seif CUF Washtukiwa
Jumuiya ya Wanawake wa Chama cha Wananchi (JUKECUF) imesema kuwa kuna mkakati wa chini kwa chini ndani ya upande wa Prof. Lipumba wa kuandaa mkutano mkuu iliouita ni bandia kwa ajili ya kumvua uanchama, Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Shariff Hamad.

Hayo yalisemwa jana na Mwenyekiti wa JUKECUF, Fatma Ferej alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo Vuga mjini Unguja.

Ferej alisema kwamba mkutano huo unaoratibiwa na upande wa Lipumba ni batili kwa sababu siyo kiongozi wa chama hicho na kwamba maazimio ya mkutano huo pamoja na mkutano wenye vitakuwa ni batili kwani hawana mamlaka.

Akitaja lengo kuu la kumvua uanachama Maalim Seif, Ferej alisema ni ili kuiondoa CUF katika kusimamia madai yake ya ushindi wa uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, 2015 ambao matokeo yake yalifutwa baada ya CUF kuibuka ushindi.

Aidha, jumuiya hiyo imetoa tahadhari kwa vyombo vya dola pamoja na Ofisi ya Msajili wwa Vyama vya Siasa kuheshimu maamuzi ya chama hicho kwani wajumbe wa mkutano mkuu wanafahamika kama walivyopatikana kupitia Uchaguzi Mkuu wa CUF wa mwaka 2014 na si vinginevyo.

Mkurugenzi wa Uchaguzi na Oganaizesheni, Nassor Seif aliyeteuliwa na Prof. Lipumba amejibu tuhuma hizo zilizotolewa na JUKECUF na kusema kwamba tuhuma hizo ni za uongo mtupu na kuwataka wananchi kuzipuuza.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad