Ndalichako Ashiriki Zoezi la Ufuatiliaji wa Miradi ya Elimu Mkoani Kigoma .. Atoa Neno

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Ndalichako  Ashiriki Zoezi la Ufuatiliaji wa Miradi ya Elimu Mkoani Kigoma .. Atoa Neno
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako leo ameshiriki zoezi la ufuatiliaji wa miradi ya elimu Wilayani Kibondo, mkoani Kigoma inayotekelezwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI pamoja na Wizara yake.

Akizungumza katika mkutano na baadhi ya watendaji wa serikali na washirika wa maendeleo, Waziri  Ndalichako amesisitiza kuwa dhamira ya  serikali ya awamu ya tano ni kuahakikisha elimu bora inatolewa ikiwa ni pamoja na kuboresha miundombinu ya shule.

Ndalichako amesema serikali inafarijika sana kuona wananchi wanajitolea katika kuboresha miundombinu hivyo ameahidi kuchangia mabati 100 ambayo yatasaidi kuboresha ujenzi wa shule shikizi ya Nyamilembi ambayo inajengwa kwa nguvu za  Wananchi.

"Sisi serikali tunawapongeza sana kwa kuwa dhamira ya serikali ni kuhakikisha  watoto wote wanapata elimu, na tunapenda sana watoto wote wasome bila kujali maumbile yao, sasa kwa kuwa mmeonyesha dhamira ya dhati ya kujenga shule shikizi na mimi nitawaunga mkono na ninawaahidi kuwaletea mabati 100", alisema Ndalichako.

Waziri Ndalichako amesema Ziara hiyo pia inalenga kubaini changamoto mbalimbali zinazozikabili shule ili ziweze kupatiwa ufumbuzi.

Kwa upande wake mkuu wa Wilaya ya Kibondo Louis Bura amesema kuwa shule shikizi ya Nyamilembi inajengwa na Wananchi kwa kuona na kutambua umuhimu wa Elimu kwa watoto wao.
Shule nyingine ambazo ujumbe huo umezitembelea ni pamoja na Shule ya msingi jumuishi  Nengo pamoja na shule ya Sekondari  wasichana Kibondo

Viongozi wengine walioshiriki ziara hiyo ni pamoja na Mkuu wa  Wilaya ya Kibond Louis Bura, baadhi ya watendaji kutoka Tamisemi, Wizara ya Elimu, wadau wa Elimu, na washirika wa Maendeleo wakiwemo SIDA na DFID.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad