AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Waziri wa Ofisi ya Rais anayeshughulikia Jiji la Kampala, Bety Kamya akisoma salamu za rambirambi kutoka kwa Rais Museveni amesema licha ya kutoa pole kwa familia, kiongozi huyo ameagiza uchunguzi wa sababu za ajali ufanyike.
Amesema pia amewapongeza maharusi, Dk Aneth na Dk Trease Ibingira na amewatakiwa maisha mema ya ndoa.
Mbali ya hilo, amesema anawaombea ili kukabiliana na kipindi kigumu walichonacho.
Amesema Rais anawashukuru Watanzania kwa kuwa wavumilivu katika kipindi kigumu cha kupoteza wapendwa wao.
"Nakabidhi vyeti hivi vya vifo vya ndugu zetu 13 nawapa pole sana," amesema Waziri Kamya akimkabidhi vyeti hivyo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angellah Kairuki.
Waziri Kairuki amesema Rais John Magufuli amepokea taarifa ya vifo hivyo kwa mshtuko na alitoa maelekezo ya kupokewa miili hiyo, kuhifadhiwa kwenye Hospitali ya Jeshi Lugalo, kuagiwa hapo na kusafirishwa kwa maziko.
Amesema maagizo hayo wanaendelea kuyatekeleza ikiwa ni pamoja na kutoa magari kwa ajili ya kusafirisha miili hiyo.
Waziri Kairuki amesema kwa namna isiyo katika wakati wa kawaida, anawapongeza maharusi na kuwatakia maisha mema.
"Haya ni mapenzi ya Mungu, hili lisiwanyong'onyeshe maharusi," amesema Kairuki.
Ameishukuru Serikali ya Uganda kwa kukodi ndege kuirudisha nyumbani miili hiyo.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK