Raila Odinga Aichachamalia Tume ya Uchaguzi Kenya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Muungano wa upinzani nchini Kenya NASA, umedai kutaka mabadiliko yafanyike ndani ya Tume ya Uchaguzi na Mipaka, IEBC, kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mpya wa urais.

Kiongozi wa upinzani Raila Odinga, amesema Tume ya Uchaguzi haiaminiki na haiwezi kusimamia Uchaguzi utakaokuwa huru na haki kama Mahakama Kuu ilivyoagiza.

Kauli ya Odinga imekuja baada ya kuanza kwa kampeni zao za kwanza jijini Nairobi leo kutokana na uamuzi uliotolewa na Mahakama ya Juu Ijumaa iliyopita ambapo ilibatilisha matokeo ya ushindi wa Uhuru Kenyatta .

Pamoja na hayo Odinga amekosoa kauli ya Rais Kenyatta ya kuwashtumu Majaji kwa kudai kuwa upinzani hawataki uchaguzi lakini wanataka serikali ya muungano, madai ambayo Odinga amepuuzilia mbali na kusema hawawezi kushirikiana na wezi wa kura.

Kenya inaelekea kwenye Uchaguzi mpya ndani ya siku 60 baada ya Mahakama ya Juu kufuta ushindi wa rais Uhuru Kenyatta kwa kubaini kuwa, haukuwa huru na haki.

Kenya imekuwa nchi ya kwanza, barani Afrika kufuta matokeo ya uchaguzi wa urais na kuingia katika vitabu vya historia.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad