Vituo vya Mitihani ya Darasa la Saba Vitakavyofanya Udanganyiu Kukiona- NACTE

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Vituo vya Mitihani ya Darasa la Saba Vitakavyofanya Udanganyiu  Kukiona- NACTE
BARAZA la Mitihani Tanzania (NECTA), limetishia kuvifutia usajili vituo vyote vya kufanyia mitihani ya Darasa la Saba inayotarajiwa kufanyika kesho Jumatano Septemba 6 na Alhamisi, Septemba 7, 2017 nchini kote.

Hayo yamesemwa leo na Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk. Charles Msonde wakati akizungumza na wanahabari Makao Makuu ya NECTA, Mikocheni jijini Dar es Salaam.

“Baraza linawataka wamiliki wa shule zote kutambua kuwa shule zao ni vituo maalum vya kufanyia mitihani, hivyo hawatakiwi kwa namna yoyote kuingilia majukumu ya wasimamizi wa mitihani hiyo.

“Baraza halitasita kukifuta kituo chochote cha mitihani endapo litabaini na kuthibitisha pasina shaka kuwa kituo hicho kinajihusisha na udanganyifu wa mitihani. Tunatoa wito kwa jamii kutoa ushirikiano kwa kipindi hiki cha ufanyikaji wa mitihani ili wanafunzi wafanye kwa utulivu.

“Tunawaasa walimu, wamiliki wa shule, wasimamizi na jamii kwa ujumla kutojihusisha na udanganyifu wa aina yoyote. Wataokiuka haya hatutasita kuwachukulia hatua kwa mujibu wa sheria za nchi,” alisema Msonde.

Awali alieleza kuwa wanafunzi hao watafanya masomo matano ambayo ni: Kiswahili, Hisabati, Maarifa ya Jamii, Sayansi na English ambapo mitihani hiyo imeshasafirishwa kupelekwa vituoni.
   
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad