AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Zitto amebainisha hayo kupitia ukurasa wake maalum wa facebook baada ya kupita siku moja tokea aliyekuwa Kaimu Mwenyekiti wa (CUF) Jimbo la Mto Pepo na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa (CUF) Wilaya ya Magharibi A. Zanzibar, Ali Juma Suleiman kufariki dunia katika hospitali ya Mnazi Mmoja kutokana na kile kinachoelezwa kuwa alivamiwa nyumbani kwake na kupigwa kisha baadaye kutupwa.
"Kuuawa kwa ndugu Ali Suleiman, Katibu wa Habari na Uenezi CUF, Wilaya ya Magharibi ni tukio lingine la kulaaniwa vikali. Kukalia kimya matukio ya namna Hii ni kukaribisha siasa ya damu kuzoeleka katika nchi yetu", amesema Zitto.
Pamoja na hayo Zitto ameendelea kwa kusema "Uchunguzi wa kina ufanyike kukomesha matukio ya namna hii, hakuna damu ya mtanzania inapaswa kumwagika kwa sababu ya siasa. Nawapa pole ndugu zetu wa CUF na wanazanzibar kwa msiba huu", amesisitiza Zitto.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK