Kidato cha Nne Waanza Kufanya Mtihani wa Taifa Leo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kidato cha Nne Waanza Kufanya Mtihani wa Taifa Leo
WATAHINIWA wapatao 385,938 wameanza kutafanya mitihani ya Taifa ya Kidato cha Nne leo Jumatatu, Oktoba 30, 2017 kote nchini. Akizungumza jana Jumapili, Oktoba 29,2017 Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta), Dk Charles Msonde alisema kati ya watahiniwa hao, 323,513 (School candidates) ni wa shule na 62,425 ni wa kujitegemea (Private candidates).
Dk Msonde alisema mitihani hiyo itaanza leo Oktoba 30, 2017 na kumalizika Novemba 17, 2017 huku akieleza kuwa maandalizi ya mitihani yameshakamilika na mitihani imeshafika kwenye vituo.
Aidha Msonde alizitaka kamati za mitihani za mikoa na halmashauri kuhakikisha utaratibu wa uendeshaji wa mitihani hiyo unafuatwa huku akiwataka wanafunzi kuacha vitendo vya udanganyifu wakati wa kufanya mitihani kwa kuwa wanaweza kufaulu bila kufanya hivyo.
“Mliyojifunza yanatosha fanyeni mitihani kwa kufuata utaratibu uliowekwa, baraza halitasita kuwafutia mitihani wote watakaojihusisha na udanganyifu, wasimamizi wa mitihani wajiepushe na vitendo vya udanganyifu, atakayekiuka atachukuliwa hatua za kisheria.” alisema Msonde.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad