Kwa Mara ya Kwanza Dogo Janja Afunguka Kuhusu Ndoa Yake na Irene Uwoya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kwa Mara ya Kwanza Dogo Janja Afunguka Kuhusu Ndoa Yake na Irene Uwoya
HABARI zilizoenea katika mitandao ya kijamii ni kwamba msanii wa muziki wa Hip Hop nchini, Dogo Janja, amefunga ndoa kimyakimya na mnyange wa filamu, Irene Uwoya.
Baada kuenea kwa uvumi huo, mtandao wa Global Publishers ulifuatilia kujua ukweli juu ya ndoa hiyo iliyowashitua wengi.

Hatua ya kwanza jana ni pale mwandishi wa mtandao alipowaendea wahariri wa Magazeti Pendwa ya Global Publishers yanayohusiana na habari za wasanii wa Bongo Muvi, Bongo Fleva na wengineo ambapo walijibu kwamba walikuwa wamemtafuta msanii Hamad Aly ‘Madee’ aliyewajibu kwamba alikuwa hajui chochote kuhusu suala hilo.

Msanii wa muziki wa Hip Hop nchini, Dogo Janja.
Mambo hayakuishia hapo kwani wahariri haohao walipowasiliana na Dogo Janja alijibu kwamba na yeye hakujua kinachoendelea.
Mwishoni wahariri wakamalizia kwa kuongea kwenye simu na Irene Uwoya ambapo alipopokea aliulizwa kuhusu suala hilo la kufunga ndoa na Dogo Janja.  Jibu la kwanza la mrembo huyo lilikuwa ni: “Mimi ni wa kuolewa?  Na nitaolewa na nani?  Na iweje niolewe na nyie Global msijue?”

…Alichokisema Madee kwenye akaunti yake ya Instagram.
Baada ya kuyasema hayo, muigizaji huyo mahiri wa filamu alimalizia kwa kusema kwamba yote hayo yalikuwa ni muvi ambayo alisema itatokea hivi karibuni.
Leo, Jumapili, mwandishi wa mtandao wetu aliwatafuta tena Madee, Dogo Janja na Irene Uwoya ili kujua iwapo walikuwa wanaendelea na msimamo wao kama walivyowaambia wahariri wetu.
Mambo yalianzia kwa Madee aliyesema ni kweli Dogo Janja amefunga ndoa ila hakutaja alikuwa amefunga ndoa na nani.  Mwanamuziki huyo aliye na makazi yake Manzese jijini, alimalizia kwa kuupa mtandao huu namba za simu za Dogo Janja ili uongee naye.

Irene Uwoya akiwa katika pozi.
Kilichofuatia ni mtandao kumpigia  simu Dogo Janja aliyeipokea na kubadilishana salam na mtandao huu lakini ghafla alinyang’anywa simu na Uwoya aliyesema kwamba ni kweli ‘bwana mdogo’ huyo alikuwa ameoa.
Hata hivyo, hakutaja kama ni yeye aliyekuwa ameolewa, lakini aliongeza kwamba: “Tafadhali tuacheni msitusumbue!”
Mpaka tunakwenda mtamboni, maelezo ya wahusika wote yalikuwa hayajaonyesha moja kwa moja kwamba ndoa hiyo kweli ilikuwa imefungwa baina ya wawili waliotajwa.
Chanzo Global Publishers
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad