Nassari Awajibu Takukuru, 'Sitokaa Kimya Endapo Sioni Hatua Zinazochukuliwa'

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Nassari Awajibu Takukuru, 'Sitokaa Kimya Endapo Sioni Hatua Zinazochukuliwa'
Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari amesema kuwa hatokaa kimya endapo haoni hatua zinazochukuliwa.

Nassari amesema hayo leo Jumanne muda mchache baada ya Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Valentino Mlowola kumtaadharisha Nassari kuacha kugeuza taarifa anazoziwasilisha kwenye taasisi hiyo kuwa ni za kisiasa.

Hata hivyo Nassari amesema, “Mlowola inabidi asome sheria ya ‘Whistle blower’ ili nikae kimya lazima nione jitihada zinazofanyika kama hakuna nitaendelea kuongea. Sitokubali kutishwa ili nisiendelee kupeleka ushahidi ninachotaka kuona ni wahusika wanachukuliwa hatua sio madiwani, wahusika wakuu ni mkuu wa wilaya na mkurugenzi,”

Awali akizungumza leo Jumanne asubuhi, Mlowola ametoa tahadhari hiyo kwa Nassari leo Jumanne, Oktoba 17, 2017 alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Amesema endapo Nassari ataendelea kuingiza siasa kwenye suala hilo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Mlowola amesema kitendo cha mwanasiasa huyo kuweka hadharani taarifa za uchunguzi ni kinyume cha sheria kwa kuwa kazi hiyo inatakiwa kufanyika kwa siri na Mahakama ndiyo yenye jukumu la kuchukua hatua.

Amesema Takukuru ina wajibu wa kumlinda mtoa taarifa lakini jukumu hilo linakuwa tofauti kwa Nassari ambaye ameamua kujitokeza hadharani.

Soma: Takukuru yamtaka Nassari kuacha kuingiza siasa katika taarifa zake

"Alicholeta Nassari kwetu ni taarifa si ushahidi. Ameleta tumezipokea na tunazifanyia kazi, inashangaza anapozungumza na vyombo vya habari na kutuelekeza namna ya kufanya kazi," amesema.

Mlowola amesema, "Tulishampa angalizo kuwa mambo tunayoongea ni siri lakini mwenzetu inaonekana anafanya siasa kama anavyosema mwenyewe kuwa ataendelea kuleta ushahidi kama series ya Isidingo."

Mkurugenzi mkuu huyo amemtaka Nassari kuacha kukiingiza chombo hicho kwenye siasa ili kifanye kazi kwa uhuru kama sheria inavyoelekeza.

"Nitoe rai kwa Nassari na wengine wote, ukishaleta taarifa kwenye chombo husika kama hiki kiache kifanye kazi. Hakuna sababu ya kukishinikiza au kukiingiza kwenye malumbano ya kisiasa. Ukweli wa mambo utajulikana mahakamani," amesema.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. mbona umejiipiga picha nyingi?
    kwa alumelu hakuna studio.
    au unafikiri zutapotea usipo zibandika zote!!
    Hebu niambie jumla ulizipiga picha ngapi...!!!?????

    ReplyDelete

Top Post Ad