AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Imetokea hitilafu gridi ya taifa na kusababisha umeme eneo lote la Dar es Salaam na baadhi ya mikoa kukosa umeme.
Tatizo hili linashughulikiwa na umeme utarudi baada ya muda mfupi
=======
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)
TAARIFA YA KUTOKEA KWA HITILAFU KATIKA GRIDI YA TAIFA
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu Wateja wake waliounganishwa katika Mikoa iliyo katika Gridi ya Taifa kuwa majira ya Saa 12:30 imetokea hitilafu kwenye Gridi ya Taifa na kusababisha Mikoa hiyo kukosa umeme.
Jitihada zimefanyika ili kurejesha umeme na baadhi ya Mikoa imeshaanza kupata huduma ya umeme
Tutaendelea kuwapa taarifa zaidi.
TANESCO inaomba radhi kwa usumbufu unaojitokeza.
Tafadhali usishike wala kukanyaga waya uliokatika au kuanguka.
Toa taarifa kupitia namba za simu zifuatazo
Kituo cha miito ya simu Makao Makuu 0222194400 na 0768 985100
Tovuti: www.tanesco.co.tz
Mitandao ya Kijamii
www.facebook/twitter.com/tanescoyetu
Imetolewa na:-
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu
25/10/2017
=======
UPDATE: Oktoba 26, 2017
Tunapenda kuwataarifu Wateja wetu waliounganishwa katika Mikoa iliyo katika Gridi ya Taifa kuwa leo Alhamisi Oktoba 26, 2017 majira ya Saa 12:03 Asubuhi imetokea hitilafu tena kwenye Gridi ya Taifa na kusabisha Mikoa hiyo kukosa umeme.
Mafundi wanafanya jitihada usiku na mchana ili kuhakikisha hali hii haijirudii na umeme unarejea katika hali ya kawaida kwa haraka
Tutaendelea kuwapa taarifa zaidi...
TANESCO
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK