Mamba Mweupe Mwenye Umri Mkubwa Aonekana Mtoni

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mamba Mweupe Mwenye Umri Mkubwa Aonekana Mtoni
Kuonekana kusiko kawaida kwa mamba mweupe mwenye umri mkubwa kumewasisimua wanaofanya shughuli za utalii katika eneo la Kaskazini mwa Australia.

Mnyama huyo wa jamii ya wanyama watambaao , aliyepewa jina la bandia -Pearl, alionekana katika ziwa Adelaide River katibu na eneo la Darwin siku ya Jumapili

Mtu mmoja aliyemuona, ambaye ni mwanaharakati wa hifadhi ya mazingira , alikadiria kuwa mamba huyo alikuwa na urefu wa mita takriban 3 za urefu.

Muonekano wa weupe wa rangi wa mnyama huyo umetokana na hali ya hypomelanism - inayosababishwa na ukosefu wa madini ya mwili yanayotengeneza ngozi melanin, kulingana na wataalam wa masuala ya wanyama..

Wakazi wa eneo lililo karibu na mto Adelaide wanaamini mnyama huyo ana uhusiano na mamba mwingine anayefahamika kuwa na hali hiyo ya afya ya mwili ambaye aliwahi kumuua mvuvi mnamo mwaka 2014.

"Kila mmoja anaelezea furaha yake ," alisema rais asiye rasmi wa kikundi cha uhifadhi wa mazingira katika eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina moja kama Broady.
"Nilishinda siku nzima nikitokwa na machozi ya furaha nikimtazama."

Muwindaji alaliwa na kuuwawa na ndovu Zimbabwe
Mamba mkubwa Big Daddy kufanyishwa ndoa Mombasa
Alama ya SOS huenda ikapata ufumbuzi Australia


Ni Kwanini mamba ni mweupe?

Wengi miongoni mwa mamba nchini Australia wanarangi za kijivu na kijani, jambo linalowawezesha kutoonekana kwa urahisi



Hitilafu ya kimwili ya Mamba Pearlhuenda ilistokea kupitia Jeni ama wakati wa kutengenezwa kwa yai , alisema Adam Britton, mtafiti msaidizi katika chuo kikuu cha Charles Darwin University.

"Wakati wa kutotoa kama mayai yatakuwa moto zaidi kiasi , inaweza kusababisha hitilafu katika kitengo cha seli na hivyo kusababisha kumeguka ," Alisema Bwana Britton.

Alisema matokeo yake yanaweza kuwa ni pamoja na "kuondolewa kwa rangi ya mwili au sehemu nyingine ya magamba kwenye mwili ".

Ni hali ya nadra ?

Mamba hao si " ni wa kawaida kuonekana'' wakiwa na umri mdogo wanapokuwa na umri mdogo, hususan katika hifadhi ya mamba, kwa mujibu wa Bwana Britton.

However, it is difficult for a pale juvenile to steer clear of predators.



"Ni jambo lisilo la kawaida kidogo kumuona mamba mwenye umri mkubwa akiwa na rangi nyeupe kiasi hicho ," Bwana Britton alisema.

"Nimeisha waona mamba kama huyu kila mara, lakini si mkubwa kiasi hiki mwituni
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad