Nipo Mbioni Kupata Mtoto Nataka 2018 Niitwe Mama- Gigy Money

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Nipo Mbioni Kupata Mtoto Nataka 2018 Niitwe Mama- Gigy Money
Msanii wa muziki ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Nampa Papa’, Gift Stanford maarufu kama Gigy Money, amedai kuwa yupo mbioni kupata mtoto, baada ya mastaa mbalimbali kufanikiwa kupata watoto hivi karibuni.

Msanii huyo anayefanya vyema na kibao chake hicho, amesema amefikia wakati wa kuitwa mama na Mungu akipenda mwakani anatamani hilo litimie.

“Kuitwa mama ni baraka na hakuna mwanamke ambaye hatamani hilo, kikubwa ni mipango tu kwa kuwa huwezi kukurupuka, halafu kingine mtoto ni mipango ya Mungu, unaweza kupanga hivi ikawa vile, sasa naona na mimi ni wakati wangu wa kutimiza hilo,” Gigy aliliambia Gazeti la Mtanzania.

Alisema pamoja na malezi kuwa na changamoto zake lakini ni jambo ambalo lazima alipitie na amejipanga vyema kutimiza azma yake hiyo aliyojiwekea na mpenzi wake.

Gigy alisema anatarajia kupata mtoto na mpenzi wake wa siku nyingi ambaye wote kwa pamoja wameridhia jambo hilo.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad