Hii ndio zawadi ya Manara kwa Papii Kocha baada ya kutoka jela

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Jumamosi ya December 9 2017 ni siku ya furaha kwa watanzania na wapenzi wa muziki wa dansi kwa ujumla, hiyo inatokana na Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kutangaza msamaha kwa wafungwa wakiwemo msanii Nguza Viking maarufu kama Babu Seya na Mwanae Papii Kocha.

Rais Magufuli ametangaza msamaha kwa Babu Seya na mwanae Papii Kocha akiwa mjini Dodoma katika maadhimisho ya miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania na muda mchache baada ya taarifa hizo kutoka watu mbalimbali tumeona wakioneshwa kufurahishwa na uamuzi huo wa Rais Maguli.

Mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa club ya Simba Haji Manara ni moja kati ya watu waliooneshwa kufurahishwa na maamuzi hayo na kaamua kuandika hivi kupitia ukurasa wake wa instagram katika picha ya Papii Kocha akiwa kavaa jezi ya Simba.

“Nchi imezizima sababu yenu . Mungu ametenda miujiza kupitia kwa Rais wetu..uliitangaza Simba hadi gerezani..ntakuvalisha jezi mpya iliosainiwa na wachezaji wote🙏🙏…ila Wenger bado hajatwaa taji…. kama ulivyomuacha🙇🙇”>> Haji Manara

Huo ni ujumbe wa Haji manara kupitia ukurasa wake wa instagram, kama utakuwa unakumbuka vizuri Babu Seya na watoto wake watatu akiwemo Papii Kocha walihukumiwa kifungo cha maisha jela mwaka 2004 baada ya kukutwa na hatia ya kesi ya kubaka na kunajisi watoto 10.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad