AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Imekuwa ni mazoea ifikapo mwishoni mwa mwaka, kituo cha mabasi yaendayo mikoani Ubungo (UBT) huwa na abiria wengi wanaosafiri kwa ajili ya sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya.
Kutokana na wingi wa abiria, baadhi ya wamiliki wa mabasi huongeza nauli; huku kukiwa na ulanguzi wa tiketi na utapeli.
Akizungumza na MCL Digital leo Jumatano Desemba 14,2017 mratibu wa idara ya barabara wa chama cha kutetea abiria (Chakua), Maulid Masaru amesema wamejipanga kukomesha utapeli, ulanguzi wa tiketi na kupandishwa nauli kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) na Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani.
"Maofisa wetu wanazunguka ndani na nje ya kituo kukagua na kuchunguza kama kuna utapeli unafanyika," amesema.
Amesema tangu Desemba Mosi,2017 hadi leo hawajapokea kesi ya utapeli au abiria kupandishiwa nauli.
Masaru amesema nauli haijapanda na abiria wanasafiri kwa nauli ya chini huenda ni kutokana na hali ngumu ya maisha.
Ofisa wa Sumatra ambaye hakutaka jina lake litajwe kwa kuwa si msemaji wa mamlaka hiyo aliyezungumza na MCL Digital, amesema hali ya usafiri si mbaya na hakuna abiria wanaoshindwa kusafiri.
Amesema wanatarajia wiki ijayo idadi ya abiria itaongezeka zaidi.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK