"Dawa ya Muhuni ni kuwa Muhuni zaidi" -Mwenyeti wa Chadema BAVICHA Afunguka

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema, BAVICHA, Patrick Ole- Sosopi amekiri kuwa Chama chake kimeamua kurudi kwenye uchaguzi mdogo haswa wa Kinondoni na Siha kwa kuwa wagundua dawa ya muhuni ni kuwa muhuni zaidi.


Akizungumza kwenye Kampeni za kumnadi Mgombea Ubunge wa Kinondoni Salum Mwalimu Ole-Sosopi amesema kwamba kilichowafanya kususia uchaguzi mara ya kwanza ni kwamba hakukuwa na faida kubwa ya kupatikana kiongozi kwa wananchi wasio na hatia kwa kumwaga damu.

Ole-Sosopi amesema kwamba baada ya kususia uchaguzi ambao uligomewa kupelekwa mbele sasa wagundua kuwa "dawa ya muhuni ni kuwa muhuni zaidi hivyo ifahamike na iwekwe rekodi kuwa CHADEMA tumerudi na kushiriki na kufanya uchaguzi".

Mbali na hayo Ole-Sosopi ameongeza kuwa hataki chama chake au kingine kisipendelewe bali waachwe wabishane kwa hoja na mwishowe wananchi waachiwe kufanya maamuzi.

CHADEMA walitangaza kugomea uchaguzi mdogo uliofanyika January 13 kwa madai mbalimbali ikiwepo kufanyia hujuma za wazi katika uchaguzi uliofanyika Novemba 26 huku tume ikilalamikiwa kutofanyia kazi malalamiko hayo.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Sosopi... Ukizidi Uhuni siku hizi... Ile Kitu itapiga shoti halafu Virusi inaingia.. Kwisha Habari.!!!
    Halafu sisi tunazika..!!!

    ReplyDelete

Top Post Ad