DC Kula Sahani Moja na Wanaopiga Wake zao

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela amepiga marufuku vitendo vya wanaume walio kwenye ndoa kupiga wake zao, akisema watakaobainika hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni wa madarasa ya shule ya Sekondari Tagamenda wilayani hapa, Kasesela amesema kuwa amechukua uamuzi huo baada ya familia nyingi kuchukulia vitendo hivyo kama jambo la kawaida.

Alisema hadi sasa ameshawachukulia hatua za kisheria wanaume zaidi ya watatu na kuwataka wanawake kuacha kuchukulia vitendo hivyo kama sehemu ya maisha yao na kuwataka kuripoti ili waweze kusaidiwa na pia kutokomezwa kwa vitendo hivyo vya kiuonevu.

" Ninatangaza hakuna mafanikio yanayoweza kupatikana ndani ya familia kama Baba na Mama hawana maelewano mazuri, na mimi sitaki kubeba dhambi za mtu yeyote atakayempiga mkewe mimi nitapambana nae," alisema Kasesela.

Hatua hiyo ya Mkuu huyo wa Wilaya ilipokelewa kwa shangwe na wakina mama wengi ambao walisema sasa amani itarejea ndani ya familia zao kutokana na wanaume wao kuwapiga hivyo sasa wanaamini furaha itakuwepo na mafanikio yatapatikana.

Pia Kasesela aliwataka wazazi hao kuwafundisha maadili yaliyo mema watoto wao ili waweze kujitunza na kuepuka maambukizi ya magonjwa ukiwemo UKIMWI.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad