AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Taarifa iliyotolewa jana na Ofisi ya Waziri Mkuu imesema mtendaji huyo mkuu wa Serikali alisema licha ya Serikali kutoa Sh600 milioni Aprili mwaka jana kwa ajili ya kuanza ujenzi wa ofisi hizo, hadi sasa hakuna kilichofanyika.
Hata hivyo, meneja huyo katika alisema maelezo yake alieleza kuwa hadi kukamilika ujenzi wa ofisi hiyo utagharimu Sh3 bilioni na kwamba kati ya fedha zilizotolewa na Serikali, Sh400 milioni zimetumika kujengea msingi, kauli ambayo ilipingwa na mkuu wa wilaya hiyo, Anna-Rose Nyamubi.
“Waziri Mkuu si kweli kwamba kuna kazi inayoendelea, bali kilichopo pale ni mashimo ambayo hayajulikani ni ya nini. Pia, kuna jengo moja lilijengwa kwa mabati kama stoo hakuna mafundi wanaoendelea na kazi,” alisema Nyamubi.
Majaliwa alisema Serikali ipo katika mchakato wa kuboresha mazingira ya wafanyakazi, ikiwamo ujenzi wa ofisi za watumishi na kwamba haitamvumilia mtu yeyote atayekwamisha juhudi hizo.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemuagiza kaimu katibu tawala wa Mara, Raphael Nyanda kutuma timu ya wakaguzi kufanya ukaguzi maalumu katika ofisi ya mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama.
Alisema halmashauri hiyo imekuwa na tabia ya kutumia fedha za miradi ya maendeleo kwa shughuli nyingine.
Alikuwa akizungumza na watumishi na madiwani wa Butiama katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Mwalimu Nyerere.
Pia, Waziri Mkuu aliagiza kuchunguzwa kwa Solomon Ngiliule, ambaye ni mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Masanja Sabuni (mweka hazina) na Robert Makendo (ofisa ununuzi).
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
HAWALIZIKI NA MISHAHARA MPAKA WAFANYE UFISADI DAH
ReplyDelete