Shilole Achoshwa na Wanaomdhalilisha Mitandaoni

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Msanii wa muziki nchini Tanzania, Zuwena Mohamed 'Shilole' amefunguka na kusema kuwa amechoshwa na mtu ambaye anajiita na kutumia jina la mume wake Uchebe na kumchafua kwenye mitandao ya kijamii kwa kuweka posti za kumdhalilisha mumewe.

Shilole amesema hayo kupitia mtandao wake wa Instgram na kudai kuwa Uchebe feki huyo amekuwa akiharibu muonekane wa mume wake kwa jamii kutokana na jumbe mbalimbali ambazo anaziweka kwenye mtandao huo.

"Plzzz plzzz nimechoka na huyo uchebe feki 'walah' ananiharibia muonekano wa mume wangu maana hana maneno haya lol! Mashabiki wangu naomba muipuuze hii acount! Acount ya mume wangu ni @uchebe1 hana fans wala nini" aliandika Shilole

Mbali na Shilole Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Klabu ya Simba SC, Haji Manara pia ameonekana kukerwa na jambo hilo na kusema kuwa anashindwa kuelewa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwanini inashindwa kuchukua hatua kwa watu ambao wanatumia majina ya watu wengine kwenye mitandao ya kijamii na kuwachafua watu kwa kuwa hata yeye pia amekuwa akifanyiwa mchezo kama huo ambao mume wa Shilole Uchebe anafanyiwa.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad