AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Vanessa amebainisha hayo wakati alipokuwa akizungumza kwenye kipindi cha eNewz kutoka EATV baada ya muda mchache kupita tokea alipomaliza kufanya mapitio ya albamu yake iliyopewa jina la 'Money Monday' na kusema amesikia kelele nyingi kwa baadhi ya wasanii kwamba albamu bongo haiuzi.
"Nimefanya 'research' kwa muda mrefu sana na nimekugundua kwamba hakuna mfumo unao-support mauzo ya albamu lakini nikasema kama ninataka kukamilika kama msanii huko ninapoelekea na vitu ninavyotegemea kufanya sitaweza kuvikamilisha bila ya kuwa na 'CV' ya kusema kwamba nami nina albamu", alisema Vanessa.
Pamoja na hayo Vanessa ameendelea kwa kusema "mwisho wa mwaka huu 2018 nategemea kuachia nyingine jumla nitakuwa nazo mbili 'so' sijaweka uoga mbele nimeweka vitendaji kazi, 'i want people to see' nina uwezo wa kufanya vitu vingi na nimefanya 'risk'kwa sababu bado sijajua kama itanilipa lakini mpaka sasa hivi naona kama malipo yapo".
Kwa upande mwingine Vanessa amewashauri wasanii wenzake waache kusikiliza kelele za watu zinazodai kuwa albamu bongo hazifanyi vizuri huku akiwaomba mashabiki wake kuendelea kumpa ushirikiano wa kununua kazi yake hiyo ambayo inauzwa kwa njia ya mitandaoni na mkononi.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK