Wagombea Kinondoni na Siha Wanasubiria Kuapishwa Tu na Kuingia Bungeni - Polepole

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wagombea  Kinondoni na Siha Wanasubiria Kuapishwa Tu na Kuingia Bungeni - Polepole
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amefunguka na kusema kuwa wagombea wa Ubunge kupitia chama chake katika uchaguzi wa marudio katika majimbo ya Kinondoni na Siha wanasubiri kuapishwa tu na kuingia bungeni.


Polepole amesema hayo alipokuwa akihojiwa na moja ya kituo cha habari na kusema kuwa kwa jinsi ambavyo wana CCM wamefanya kazi nzuri sana Kinondoni na Siha kuhakikisha wanawanadi na kuwauza wagombea wao hivyo wana uhakika wa kushinda uchaguzi huo kwa kishindo.

"Kwa utafiti tunaofanya na kazi nzuri tuliyofanya tunasubiri kutangazwa washindi katika majimbo yote mawili pale Kinondoni na Siha" alisisikika Polepole akisema

Mbali na hilo Polepole amekanusha chama hicho kuwa na mvurugano wa wenyewe kwa wenyewe kufuatia kusimamisha wagombea katika majimbo hayo ambao hawana muda mrefu katika chama hicho wakitokea upinzani na kusema kwa CCM kila mwanachama ana haki sawa na wanachama wengine.

Chama Cha Mapinduzi kimemsimamisha Maulid Mtulia kugombea Ubunge kwa jimbo la Kinondoni wakati katika jimbo la Siha kimemsimamisha Dk Godwin Mollel ambao wote walikuwa ni wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutokea vyama vya upinzani, lakini walijivua uanachama kwenye vyama vyao na kujiunga na CCM.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad