Wanasheria Wamuunga Mkono Makonda Kuwasaidia Waliodhulumiwa Mali Zao

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wanasheria Wamuunga Mkono Makonda Kuwasaidia Waliodhulumiwa Mali Zao
Dhamira njema ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda kuamua kuwasaidia wanyonge walioteseka na kunyanyasika muda mrefu baada ya kudhulumiwa Mali zao walizochuma kwa Jasho imewafanya Wanasheria kuguswa na kuamua kujitokeza kusaidia jitiada hizo ili kuhakikisha haki ya mnyonge inapatikana pasipo kuvunja Sheria.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akizungumza na wananchi hao.

RC Makonda amesema idadi ya Wanasheria imeongezeka kutoka 160 hadi kufikia 246 siku ya leo ambapo ameshukuru Uongozi wa Shule ya Wanasheria kwa Vitendo (Law school), Mawakili wa kujitegemea pamoja na Chama cha Mawakili (TLS) kwa kumuunga mkono na kuwaomba wanasheria wengine kujitokeza kuwasaidia wananchi.

Aidha RC Makonda ameshukuru jopo la wanasheria wanaohudumu kwenye Zoezi hilo kwa umakini na huduma nzuri wanayotoa kwa wananchi waliojitokeza kitendo kinachowapa faraja wananchi ambao wametaabika kwa miaka mingi kutafuta haki yao.

RC Makonda amesema lengo lake ni kuhakikisha kila mwananchi aliefika na kupata namba anasikilizwa kwa umakini chini ya jopo la wanasheria makini wasiopungua Saba.


Baadhi ya wananchi akiwemo Mzee Paul Kiakaisho yeye anasema ameteseka kwa miaka Saba akitafuta haki baada ya kutapeliwa nyumba na alipowatafuta mawakili walimwambia ili waweze kumsimamia apate haki anapaswa kulipa million tano ambayo kwa Hali yake ngumu ya maisha Hakuwa na uwezo hivyo amemshukuru RC Makonda kutenga siku tano za kusikiliza Wananchi Bure.

Zoezi la kutoa msaada wa kisheria kwa wananchi waliodhulumiwa haki zao linaendelea hadi ijumaa ya February 02 likihusisha wenye malalamiko ya Kudhulumiwa Nyumba, Viwanja, Mirathi, Kazi, Magari,waliodhulumiwa kampuni zao,waliopata ulemavu makazini pasipo kulipwa,waliobakwa na kupoteza maisha pamoja na utapeli wa kukusanya Hati kama mkopeshaji kisha kuchukuwa mkopo Bank na kukimbia baadae Watu wanauziwa
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad