AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Sirro ametoa kauli hiyo jana Februari 21, 2018 katika ziara yake ya siku moja wilaya za Handeni na Korogwe mkoani Tanga, ambako licha ya mambo mengine alikagua majalada ya kesi, vielelezo na kuzungumza na askari kuhusu nidhamu.
Amesema askari atakayebainika kupokea rushwa na kuwabambikia watu kesi atachukuliwa hatua za nidhamu.
“Ninatembelea vituo vya polisi kukagua majalada ya kesi, kuangalia sababu za kesi kuchelewa. Pia, ninaangalia kama kuna kesi ambazo wahusika wamebambikiwa ili kuyafanyia kazi mambo haya,” amesema Sirro.
Pia, amevitaka vyombo vya dola Tanga kutoa elimu dhidi ya kesi za ubakaji na wizi wa mifugo kwa kuwa zinaonekana kukithiri na kutaka hatua stahiki zishukuliwe kwa wahusika.
“Kama kuna kubambikia watu kesi tutabaini, tukimbaini askari tutamwajibisha ndiyo maana ninapitia majalada na vielelezo kuona wanakwama wapi ili tujue kama tatizo ni ofisi ya mkemia mkuu, waseme ili tuweze kufuatilia na kumaliza hizi kesi kwa kutenda haki,” amesema.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK