Suluhu Linapatikana Mezani Nasio Maandamano- Gambo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Suluhu Linapatikana Mezani Nasio Maandamano- Gambo
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo amefunguka na kuwashukuru Chama cha wafanyakazi Tanzania (TUCTA) kwa kuweza kutatua changamoto za wafanyakazi kwa kukaa nao mezani badala ya ule utaratibu wa zamani uliozoeleka wa kuandamana.

Gambo ameeleza hayo kupitia ukurasa wake maalumu wa kijamii asubuhi ya leo mara baada ya kupata taarifa ya mkoa wake kuchaguliwa kuwa wenyeji wa shughuli za Mei mosi kitaifa 2018.

"Tunawashukuru sana kwa kutupa heshima hii ya kuwa mwenyeji wa maadhimisho haya muhimu yanayohusu wafanyakazi wetu. Nimewapongeza kwa utaratibu wenu wa kutafuta suluhu ya changamoto za wafanyakazi kwa kukaa mezani na serikali badala ya utaratibu wa kizamani wa kuandamana", amesema Gambo.

Sherehe za hizo zilizopewa jina la 'Sikukuu ya wafanyakazi' huwa zinaanzimisha kila ifikapo mwezi wa Tano tarehe moja nchini Tanzania ambapo Rais wa nchi huwa anatumia jukwaa hilo kutatua shida na kero za wafanyakazi papo kwa hapo pamoja na kutangaza kushusha au kupandisha daraja za mishahara bila ya kusahau kodi ya kichwa.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad