AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akiongozwa na mawakili Nehemiah Nkoko na Ruben Simwanza kutoa utetezi wake jana, Masogange aliiomba mahakama hiyo imuachie huru kwa sababu hana kosa lolote.
Masogange anakabiliwa na kesi ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin na Oxazepam, katika utetezi wake alidai kuwa hajawahi kutumia dawa za kulevya hata siku moja. Aliiambia mahakama kuwa mbali ya usanii, alikuwa ni mfanyabiashara wa nguo. Alieleza kuwa Februari 14, 2017 polisi walikwenda nyumbani kwake bila yeye kuwapo kwa sababu alikuwa amempeleka mjomba wake duka la Ocadeco kununua vitu, hivyo walimkuta dada yake.
Aliongeza kuwa polisi hao walimweka dada yake chini ya ulinzi na kumtaka ampigie simu na kujifanye anaumwa ili arudi nyumbani, hivyo alitii amri na baada ya kumjulisha hivyo alimuahidi kuwa atarejea nyumbani punde lakini alirudi saa 12:00 jioni.
Aliendelea kuwa alipofika nyumbani kwake getini kabla hajashuka kwenye gari, alimuona mlinzi amekaa na watu wanne, aliwasalimia na kuingia ndani lakini ilipoingia ndani alimkuta dada yake, askari wa kike na wengine wawili wa kiume, walijitambulisha kwake na kumweleza kuwa wanamsubiri.
Masogange alidai aliwauliza shida yao na walimjibu kuwa wamekwenda kufanya upekuzi, lakini hawajapata kitu chochote.
Baada ya upekuzi huo, walimpeleka Kituo Kikuu cha Polisi na walipofika mapokezi akaandikisha jina na wakampeleka rumande ambako alikaa siku tisa.
Aliongeza kuwa baada ya kukamatwa Februari 14,2017, siku iliyofuatia akiwa polisi alipelekwa ofisi iliyokuwa na watu 15 ambako kwa nyakati tofauti alikuwa wakimuuliza maswali.
Baada ya kufunga ushahidi wake, hakimu mkazi mkuu, Wilbard Mashauri alisema atatoa hukumu Februari 21.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK