Serikali Yapiga Marufuku Matangazo ya Kuongeza Makalio

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Serikali Yapiga Marufuku Matangazo ya Kuongeza Makalio
Serikali kupitia Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini Tanzania (TFDA) kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi nchini, imepiga marufuku matangazo ya biashara za vipodozi na dawa za kuongeza maumbile kwenye mitandao ya kijamii kama vile Instagram, Facebook, Twitter na kwenye blogs.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Februari 18, 2018 jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa TFDA, Agnes Kijo amesema matangazo hayo yanatakiwa kukoma mara moja na wahusika wanastahili kufika katika mamlaka hizo kuomba kibali.

Bi Kijo amesema kumekuwepo na wimbi la watu mbalimbali wanaotangaza vipodozi kwa lengo la kujichubua na dawa za kuongeza maumbile kwenye mitandao hiyo ya kijamii wakifanya kinyume na Sheria ya Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi sura ya 219.

Amesisitiza kuwa matangazo ya vipodozi na dawa hizo yamekuwa na madai mbalimbali kama vile kuongeza makalio, kuongeza nyonga, sehemu za siri za mwanaume, kurudisha bikira kwa wanawake na kuondoa mabaka sugu na tiba hizo kwenye mfumo wa vidonge, jeli, losheni, mafuta, krimu na dawa za kunywa. Kijo alisema baadhi ya watu wamekuwa wakipotosha umma kuwa bidhaa zao zimethibitishwa na TFDA kitu ambacho si kweli.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad