Watu Wawili Wakamatwa Kwa Tuhuma za Mauaji ya Kiongozi wa Chadema

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Watu Wawili Wakamatwa Kwa Tuhuma za Mauaji ya Kiongozi wa Chadema
Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es salaam limefanikiwa kuwakamata watu wawili wanaotuhumiwa kuhusika kwenye mauaji ya aliyekuwa Katibu wa CHADEMA kata ya Hananasif, aliyeuawa kwa kukatwa na mapanga na mwili wake kutupwa Coco Beach.

Tokeo la picha la kamanda mambosasa
Kamanda Mambosasa

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Februari 26, 2018. Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema watu hao ni mwanamke na mwanaume huku akikataa kuwataja majina yao ili kutoharibu ushahidi.

“Mnamo tarehe 23 Februari 2018 majira ya saa 5:30 usiku huko katika maeneno ya Hananasif, Kinondoni kufuatia uchunguzi unaoendelea juu ya mauaji yaliyokuwa yameripotiwa wamekamatwa watu wawili mmoja wa kike na mwingine mwanaume kwa tuhuma zinazohusiana na mauaji haya,“amesema Kamanda Mambosasa na kutolea maelezo juu ya majina yao.

“Nimeshindwa kuwataja majina hapa kwa sababu za kiupelelezi katika wale ambao wanafuatiliwa hapa bado wengine hatujawakamata, kwa hiyo tutaendelea kuwafuatilia ili tuweze kuwatia mbaroni,“amesema Mambosasa.

Soma zaidi – Marekani yalaani mauaji ya kiongozi wa CHADEMA

Wiki mbili zilizopita mwili wa marehemu Daniel John uliokotwa katika fukwe za Coco Beach ukiwa umejeruhiwa vibaya na mabanga sehemu za mwili wake.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad