Evans Aveva Hali Tete Alazwa ICU Muhimbili

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Evans Aveva Hali Tete Alazwa ICU Muhimbili

Rais wa Klabu ya Simba, Evans Aveva amelazwa katika kitengo cha wagonjwa mahututi Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).

Hayo yameelezwa leo Machi 8 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri na wakili anayewatetea, Evodius Mtawala wakati kesi hiyo ilipotajwa mahakamani hapo.

“Mshtakiwa wa kwanza Aveva, tangu jana amelazwa katika kitengo cha wagonjwa mahututi hali yake siyo nzuri," ameeleza wakili Mtawala.

Hata hivyo, mwendesha mashtaka wa Takukuru, Leonard Swai naye ameliambia mahakama kuwa Aveva ni mgonjwa na kwamba upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, Mtawala ameiambia mahakama kuwa walizungumza na upande wa mashtaka wataeleza jalada la kesi hiyo bado lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) na wameomba wapewe siku 14 ili waweze kueleza kitu.

Hakimu Mashauri ameiahirisha kesi hiyo hadi Machi 22, 2018.

Wakati kesi hiyo ikitajwa mahakamani hapo alikuwapo Godfrey Nyange maarufu Kaburu ambaye ni makamu wa rais wa Klabu ya Simba.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka matano ya  uhujumu uchumi ikiwamo kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha wa kiasi hicho cha fedha.

Washtakiwa hao wapo mahabusu kutokana na kukabiliwa na mashtaka ya utakatishaji fedha ambayo hayana dhamana kwa mujibu wa sheria.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad