Jeshi la Polisi Dodoma Lawashikilia Wahamiaji

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Jeshi la Polisi Dodoma Lawashikilia Wahamiaji
Jeshi la Polisi mkoani Dodoma linawashikilia wahamiaji haramu wawili raia wa Rwanda pamoja na watoto 20 wa mitaani wenye umri kati ya miaka 7 hadi 15 ambao wamekuwa wakitumiwa na wahalifu kuiba vifaa mbalimbali vya magari.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma Giles Muroto akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma  , amesema katika msako uliofanywa tangu Februari 28 mwaka huu, wamefanikisha kukamatwa kwa wahamiaji wawili na watoto hao ambao wamekuwa wakitumia dawa za kulevya aina ya gundi.

Kamanda huyo amesema wazazi wa watoto hao wanapaswa kufika kituoni kuwachukua watoto hao ili kuepusha kushtakiwa kwa mujibu wa sheria kwa kushindwa kuwalea watoto wao.

Aidha amesema pia katika msako huo jeshi hilo limewakamata wahamiaji haramu wawili februari 28, mwaka huu ambao ni raia wa Rwanda katika 'check point' ya polisi mtera wilayani Mpwapwa barabara ya kuelekea Iringa.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad