AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza mara baada ya kutembelea shule hiyo leo Machi 5, 2018 Shigela amesema ni mapema kuzungumzia chanzo cha moto huo huku akivitaka vyombo hivyo kuanza uchunguzi ili kubaini chanzo pamoja na madhara yaliyojitokeza.
“Kulitokea tatizo la umeme kuwaka na kuzima ambalo hata mkoani lilikuwepo ila hatuna uhakika, hivyo naagiza vyombo vya ulinzi na usalama kwa siku 14 kuchunguza chanzo cha tatizo na athari zake kwa wanafunzi na mali zao ili tujue,” amesema Shigella
Pia, Shigela ameagiza wadau wa elimu kuona umuhimu wa kuchangia shule hiyo kwa maelezo kuwa yanahitajika magodoro na vifaa vingine muhimu shuleni hapo ili wanafunzi waweze kuendelea na masomo yao.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Annisia Mauka amesema hakuna madhara kwa mwanafunzi yeyote kwani wakati moto unatokea wote walikuwa wanajisomea darasani.
Amesema mpaka sasa kuna bajeti ya Sh1.3bilioni kwa ajili ya ukarabati wa shule hiyo yakiwemo mabweni ila hakuna bajeti ya bati kwa ajili ya ujenzi.
Daktari wa Hospitali ya Wilaya ya Korogwe, Frank James amesema walipokea wanafunzi 43 walioonekana wazi kuathiriwa na moshi wakati bweni hilo likiwaka moto lakini walipatiwa matibabu na kuruhusiwa kurudi shuleni.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK