AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mke wa nane wa Mfalme Mswati wa Swaziland Senteni Masango, amejiua Ijumaa ya wiki iliyopita, wa kunywa dawa za vidonge aina ya amytriptyline, ambazo ndizo zilizoondoa uhai wake.
Malkia huyo amejiua wiki moja baada ya kuhudhuria mazishi ya dada yake Nombuso Masango, ambapo tetesi zinasema kwamba Mfalme alimkataza kuhudhuria mazishi hayo.
Habari zaidi zinasema kwamba mke huyo ambaye aliolewa mwaka 1999 na kuwa mke wa 8 wa Mfalme Mswati, alikuwa akiishi kwenye kasri ya Kifalme peke yake kwa takriban miaka mitatu, bila kutembelewa na mume wake huyo.
Tayari Malkia huyo wa Swaziland ambaye alikuwa miongoni mwa wake vipenzi wa Mfalme Mswati amezikwa kwenye eneo la kifalme la Swaziland, huku Mfalme Mswati akiendelea kupokea salamu za pole kwa viongozi mbali mbali wa serikai.
Habari zinasema kwamba Mfalme Mswati alishawahi kukimbiwa na wake wawili kwa tuhuma za unyanyasaji, huku wengine akiwapa adhabu kali ikiwemo kutengwa na kasri ya Kifalme.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK