Mwili wa mbunge Bilago wa CHADEMA kuagwa Jumatatu Dodoma

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema mwili wa aliyekuwa mbunge wa Buyungu (Chadema), Kasuku Bilago utaagwa Jumatatu Mei 28, 2018 bungeni mjini Dodoma.

Taarifa iliyotolewa leo Mei 26, 2018 na kitengo cha habari, elimu na mawasiliano cha Bunge, imeeleza kuwa baada ya kuaga mwili huo utapelekwa Kakonko mkoani Kigoma kwa ajili ya mazishi.

“Ofisi ya Bunge inaendelea na kuratibu taratibu za mazishi kwa kushirikiana na familia ya marehemu na taarifa zaidi zitaendelea kutolewa,” inaeleza taarifa hiyo.

Bilago amefariki dunia leo saa tisa alasiri katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.

Alihamishiwa Muhimbili Mei 22, 2018 akitokea Hospitali ya DCMC iliyopo eneo la Ntyuka jijini Dodoma alikokuwa amelazwa.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad