AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mongella ameongea hayo Juni 17, 2018 wakati wa uzinduzi wa kivuko kipya cha MV Mwanza ambacho kitafanyakazi katika eneo la Kigongo-Busisi, na kuongeza kuwa Serikali ya awamu ya tano imefanikiwa kufanya mambo makubwa katika kipindi cha muda mfupi tangu kuingia madarakani chini ya Rais Magufuli.
“Unaweza kumsema Magufuli labda hupendi sura yake, lakini huna namna ya kusema huyu mtu hafanyikazi, Serikali inapiga kazi leo tunaona meli MV Mwanza itaenda pale Kigongo feri kwenda Busisi ina uwezo mkubwa, ni jambo kubwa hii meli ni ya kisasa zaidi ni nyepesi, ina kwenda kasi na inabeba mzigo mkubwa” amesema Mongella
Mongella ameongeza kuwa kivuko hicho cha kisasa kitasaidia ufanisi katika sekta ya usafiri wa majini katika ziwa victoria kwasababu itasafirisha mizigo mikubwa kwa wakati mmoja na kwa gharama nafuu na kuwataka wananchi kuunga mkono jitihada za maendeleo zinazofanywa na Rais Magufuli.
Kivuko cha MV Mwanza kina uwezo wa kubeba uzito wa tani 250, kitafanya kazi katika eneo la Kigongo–Busisi Mkoani Mwanza na utengenezaji wake umegharimu jumla ya shilingi bilioni 8 na kitaweza kubeba abiria 1000 na magari 36 kwa wakati mmoja.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK