AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Haji Manara leo Juni 25, 2018 na kusema walichekwa na kudhalilishwa sana kwenye msimu ulioisha kwa kusajili wachezaji wazee kama watu wasemavyo lakini ndio waliowawezesha kupata ubingwa.
"Nakumbuka vema tulipowasajili hawa Wanaume (John Bocco, Emmanuel Okwi na Erasto Nyoni) jinsi tulivyodhihakiwa, waliitwa wahenga tukaambiwa tumesajili 'ICU' na maneno mengi. Tena hata baadhi ya wanasimba walitulaumu viongozi",ameandika Manara.
Pamoja na hayo, Manara ameendelea kwa kusisitiza kuwa "tulijua 'what we did' na imelipa, hao ndio wachezaji bora katika msimu huu. Hakuna ubishi na sijasikia lalamiko lolote, sasa 'for next season' pamoja na usajili tulioufanya tutaongeza wanaume. Tunayakumbuka vema maelekezo ya Mh Rais wa nchi".
Majigambo hayo ya Haji Manara yamekuja baada ya kupita siku moja tokea zilipotolewa Tuzo za Ligi Kuu Tanzania Bara na timu yake kuweza kuchukua Tuzo nyingi zaidi ya washiriki wengine waliokuwepo katika kinyang'anyiro hicho licha ya maneno mengi yaliyokuwa yanaiandama timu yake kuwa ilisajili wachezaji wazee ambao wasingeweza kuitumikia klabu ipasavyo lakini ikawa ndivyo sivyo.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK