Twaweza: Hatuhusiki Kusambaza Barua ya Costech Mitandaoni

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Twaweza: Hatuhusiki Kusambaza Barua ya Costech Mitandaoni
Muda mfupi baada ya Tume ya Sayansi na Teknolojia, (Costech) kusema wamesikitishwa na kitendo cha kusambaa mitandaoni kwa barua waliyowaandikia taasisi ya Twaweza, Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Aidan Eyakuze amesema hawajahusika kuisambaza.

Eyakuze ameyasema hayo leo Julai 12, kwenye ukurasa wa twitter wa taasisi hiyo.

“Kama tulivyosema awali, tumepokea barua kutoka Costech na tunaifanyia kazi. Twaweza haijasambaza barua hiyo wala kuhusika kuisambaza kwenye mitandao ya kijamii,” imesema taarifa hiyo

Eyakuze amesema, barua zote zinazopelekwa Twaweza huwekwa muhuri mbele ya aliyetumwa kuipeleka pamoja na risiti.

“Barua inayosambaa mitandaoni haina muhuri wetu, tunaheshimu mawasiliano yote yanayofanywa na wadau wetu,” amesema

Leo Kaimu Mkurugenzi wa Costech  Dk Amos Nungu alizungumza na wanahabari na kusema wamesikitishwa na kusambaa mitandaoni  kwa barua hiyo waliyopelekewa Twaweza
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad